Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 56 2023-09-04

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya kisasa kwenye eneo la Bondeni City Jijini Arusha kupitia Mradi wa TACTIC?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mrisho Mashaka Gambo, Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia mradi wa kuboresha miundombinu katika Majiji, Manispaa na Miji – TACTIC awamu ya pili, itatekeleza ujenzi wa stendi kuu ya kisasa ya mabasi katika eneo la Bondeni City, masoko mawili pamoja na bustani moja ya mapumziko kwa lengo la kuboresha huduma za kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa Jiji la Arusha na maeneo jirani.

Mheshimiwa Spika, kazi ya usanifu imekamilika na taratibu za ununuzi kwa ajili ya kumpata mzabuni zinatarajiwa kukamilika mwezi Disemba, 2023. Baada ya taratibu hizo kukamilika, utekelezaji wa ujenzi kwenye maeneo yaliyoainishwa utaanza, ahsante.