Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuvuna fisi wanaovamia makazi ya Wananchi, kujeruhi na kuua Watu katika Kata ya Endamarariek?

Supplementary Question 1

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. Kwanza niseme siridhiki na majibu ya Serikali kwa sababu hizo jitihada zimefanywa na wananchi na takribani watu 24 ndani ya miaka mitatu wakiwemo Watoto wameuawa na fisi. Sasa swali langu;

a) Je, ni lini na kwa uhakika hilo jeshi la uhifadhi litafika katika eneo hilo na kuwavuna fisi hao ili wananchi waendelee kukaa kwa amani?

b) Je, ni lini, Serikali itakuja na mkakati wa kutoa elimu kwa wananchi ili yanapotokea majanga kama hiyo waweze kujihami na kukabiliana na Wanyama wa namna hiyo?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kwenye swali lake la nyongeza linalohusiana na lini Jeshi la Uhifadhi litaenda kuwasaka, naomba tu niendelee kuelekeza kuanzia sasa kwamba Jeshi la Uhifadhi Kanda ya Kaskazini waelekee Karatu, wakaamnze kufanya msako wa fisi hao ili wananchi waweze kuona umuhimu wa uhifadhi lakini pia fisi hao waweze kurudishwa hifadhini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala hili la elimu. Kwa sasa hivi tumeanza programu za kufundisha au kuelimisha wananchi namna ya kujikinga na wanyama wakali na uharibifu. Kwa hiyo naendelea kuelekeza kwenye upande wa Kanda ya Kaskazini kwamba, pamoja na msako huo utakaofanyika pia watoe elimu kwa wananchi ili tuweze kuwa na mashirikiano ya pamoja.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuvuna fisi wanaovamia makazi ya Wananchi, kujeruhi na kuua Watu katika Kata ya Endamarariek?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mbali na fisi kusumbua wananchi na kuleta madhara kwa watu wenye hifadhi pia kumekuwa na tatizo kubwa la mamba katika Ukanda wa Ziwa Victoria hasa maeneo ya Tairo na Guta Pamoja na Wilaya ya Bunda upande wa Mwibala;

Je, nini tamko la Serikali katika kuhakikisha mnaenda kuvuna mamba hao?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwenye upande wa mamba tumeshaanza programu ya kutengeneza vizimba na kuwafundisha wananchi namna ya kujikinga nao. Kwa sababu tatizo linajitokeza ni pale ambapo wananchi walizoea kuogelea ziwani, wengine wana mazoea ya kwenda kucheza kandokando ya ziwa. Nakumbuka enzi za zamani hasa wale tulioishi Kanda ya Ziwa, tulikuwa tuna maeneo yetu ambayo huruhusiwi kwenda kucheza maeneo hayo kwa sababu kuna Wanyama wakali hususan mamba na viboko.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kadri tunavyozidi kuongezeka wananchi wanaendelea kuyasogelea yale maeneo. Kwa hiyo tunaendelea kuwaelimisha wananchi kama yale mazoea ya wananchi ya kila siku ya Kwenda kuogelea kama ilivyo zamani tuyaache, na matokeo yake tunatengeneza vizimba kama wanaenda kuchota maji basi waende kwenye maeneo yale.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kadri tunavyozidi kuongezeka wananchi wanaendelea kuyasogelea yale maeneo. Kwa hiyo, tunaendelea kuwaelimisha wananchi kwamba, yale mazoea ya kila siku ya kwenda kuogelea kama ilivyokuwa zamani tuyaache na matokeo yake tunatengeneza vizimba, kama wanaenda kuchota maji, basi waende kwenye maeneo yale tu ambayo yameainishwa, ili kuepuka hii athari inayojitokeza ya hasa watoto wanachukuliwa na mamba na inakuwa ni athari kwa wazazi pia na kwa jamii kwa ujumla. Kwa hiyo, tunawaelimisha wananchi pia waendelee kuyaheshimu haya maeneo.