Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 29 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 384 2023-05-19

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuvuna fisi wanaovamia makazi ya Wananchi, kujeruhi na kuua Watu katika Kata ya Endamarariek?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kukabiliana na changamoto ya fisi kuvamia maeneo ya makazi ya wananchi hususan kwenye Kata ya Endamarariek Wilayani Karatu, Wizara kupitia Jeshi la Uhifadhi pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Karatu imekuwa ikifanya msako wa fisi katika maeneo husika ambapo tangu mwaka 2019 hadi sasa jumla ya fisi saba wamevunwa. Aidha, mapango/makazi ya fisi 11 yameharibiwa katika maeneo husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa fisi wanaishi katika makundi, Wizara inaendelea kufanya soroveya ili kuyabaini makundi ya fisi yaliyosalia na kuyavunja ikiwa ni pamoja na kuharibu makazi yao.