Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, maeneo mangapi yameshabainishwa kuwa ni vyanzo vya maji salama ardhini na hatua gani zinachukuliwa kulinda maeneo hayo?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili.

Mheshimiwa Naibu spika, swali la kwanza. Kwa kuwa maji chini ya ardhi ni Pamoja na chemchem zinazofumuka wakati wa masika na kupotea wakati wa kiangazi hasa mkoani Kilimanjaro;

Je, Serikali inazitambua na kuziwekea udhibiti chemchem hizo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa utafiti wa Chuo Kikuu cha SUA kimebaini kuwa maji chini ya ardhi yanapungua sana lakini Serikali haijaweza kudhibiti maji ya mvua ya kila msimu na kila mwaka yanayotiririka na kutuharibia barabara. Serikali ina mpango gani sasa wa kufanya project ambayo itaweza kudhibiti hali hiyo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shally Raymond, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, chemchem zote za Mkoa wa Kilimanjaro ni chemchem ambazo zina manufaa makubwa katika kuongeza maji katika miradi yetu inayoenda kwa wananchi. Hivyo tunailinda na kuidhibiti na tunaitambua vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, kuhusu maji chini ya ardhi hupungua na sasa maji yanapotea. Hapa tumshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hasssan, tuna mitambo mitano ya kuchimba mabwawa na lengo la kuchimba mabwawa haya ni kuhakikisha maji yote ya mvua tuweze kuyatunza kwa ajili ya mhitaji wakati wa kiangazi. Tunataka kuonesha kwamba mvua ambazo Mwenyezi Mungu anatupatia siyo laana bali ni baraka na yanakwenda kutumika vizuri.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, maeneo mangapi yameshabainishwa kuwa ni vyanzo vya maji salama ardhini na hatua gani zinachukuliwa kulinda maeneo hayo?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kumekuwa kuna utaratibu wa uuzwaji wa maji kupitia ma – bowser ya magari kwa gharama kubwa kwa wananchi na ilihali ya Serikali imeweka mtandao mzuri sasa hivi wa maji Kibamba;

Je, Serikali mko tayari kutoa kauli ya usitishaji wa uuzaji wa maji kupitia magari?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mtemvu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, usitishaji wa kuuza maji kwenye magari, huu sio utaratibu rasmi. Tutalifanyia kazi pamoja na Wizara husika.