Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza: - Je, Wamachinga wangapi wamefuzu kuwa Wafanyabiashara rasmi kwa kipindi cha kuanzia 2016 hadi 2021?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; Serikali inakiri kwamba bado haijapata kutambua vizuri kundi hili na ilihali na yenyewe inatambua kwamba ilitoa vitambulisho;

Je, Serikali iko tayari kukiri kwamba vitambulisho vile havikusaidia kutambua kundi hili, haswa kwa teknolojia duni ambayo imetumika?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Ili machinga atoke kwenye hali ya umachinga na Kwenda katika kundi la wafanyabiashara wagodo na wa kati, ni lazima apewe afua mbalimbali za kikodi;

Je, Serikali ina mpango gani sasa kuzibainisha hizo afua za kikodi ili hawa wamachinga waweze kuzitambua na waweze kuingia kwenye kundi la wafanyabiashara rasmi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ni kweli moja ya changamoto zilizojitokeza kwa vitambulisho vile vya awali vya kuwatambua wamachinga ilikuwa ni kwamba vinaweza vikatumika na mtu yoyote kwa sababu havikuwa vya kielektroniki. Moja ya kazi kubwa tunayofanya sasa katika bajeti inayokuja ni Serikali Kwenda kutoa vitambuilisho vya kielektroniki ambavyo vitasaidia kuwatambua wajasiriamali walipo, lakini pia pale ambapo watakuwa wamekua, kwa maana kutoka mitaji ile midogo ya 4,000,000 ambayo tunatambua kama wajasiriamali, kwenda juu tutawatambua kama wafanyabiashara halali na kuwarasimisha kwenye kundi halali la wafanyabiashara kutoka wajasiriamlali.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwenye swali la pili; Serikali inafanya kazi kubwa sana. Moja ni kurasimisha kuwatambua wajasiriamali hawa na Mheshimiwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan ametoa fedha 10,000,000 kuanzisha ofisi za wamachinga kila Mkoa. Sasa kupitia hizo tutawatambua na kuwasaidia kupata mikopo nafuu kwenye taasisi zetu za fedha, lakini pia utaratibu unaokuja ni kuona zile fedha asilimia 10 ambazo zilikuwa zinatolewa ziweze kuwa na manufaa kupitia benki ili wajasiriamali hawa wadogo ambao wanahitaji mitaji kwa ajili ya kuendeleza biashara zao wanufaike.