Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 29 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 382 2023-05-19

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza: -

Je, Wamachinga wangapi wamefuzu kuwa Wafanyabiashara rasmi kwa kipindi cha kuanzia 2016 hadi 2021?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA, alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi kufikia Machi, 2023 kuna jumla ya Machinga 1,987,361 nchini. Aidha, kwa sasa Serikali inaanda utaratibu wa kuwatambua Wamachinga waliofuzu kuwa wafanyabiashara mara baada ya kurasimisha biashara zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuhamasisha urasimishaji wa biashara nchini kupitia njia mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya faida za urasimishaji biashara kupitia mafunzo mbalimbali ya biashara ya ujasiriamali. Mikakati iliyopo kwa sasa ni uanzishwaji wa vituo jumuishi vya urasimishaji wa biashara na uandaaji wa mwongozo wa taratibu za kurasimisha biashara nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.