Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: - Je, hadi sasa hali ya ugonjwa wa figo ipoje nchini?

Supplementary Question 1

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Kwanza nachukua nafasi kwa kuipongeza Serikali kwa kujengwa kwa hospitali za mMikoa;

Je, ni lini Hospitali hizo za Mikoa zitaanza huduma za dialysis?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali langu la pili. Kwa kuwa Serikali imekiri kwamba gharama za matibabu ziko juu;

Je, nini kauli ya Serikali juu ya kuwasaidia wale wananchi masikini ambao hawana uwezo wa kukidhi gharama hizo za matibabu?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge, kwa namna ambavyo anashirikiana na Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa wa Manyara kufutilia shughuli mbalimbali za afya katika mkoa huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza linahusu huduma kwenye hospitali zetu za mikoa. Kati ya bilioni 290.9 ambazo Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu amezileta zimetumika kununua vifaa kwa ajili ya dialysis kwa hospitali zote za mikoa. Na hata Mkoa wako wa Manyara vifaa tayari vimefika na nategemea mpaka sasa kazi hiyo imeanza na watu wanapata huduma pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili linahusu suala la gharama. Ni kweli ni gharama kubwa sana kwenye eneo la kutibu figo, na nilisema juzi hapa. Tunafikiri kwamba bei yake inaweza ikashuka kuanzia tisini hadi 150,000, hapo inawezekana kushusha. Lakini kuna utaratibu wa exemption kwa watu ambao wananshindwa kulipa. Kama yuko kule Manyara kwenye kata yake akiwa na barua ya mtendaji wake wa kata, akifika hospitali anastahili kutibiwa bure.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: - Je, hadi sasa hali ya ugonjwa wa figo ipoje nchini?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa matibabu ya ugonjwa wa figo nchini yakemkuwa na gharama kubwa sana na kwa kuwa bima ya afya kwa sasa haitoi huduma ya ugonjwa huu; je, ni utaratibu upi mbadala wa Serikali ili kusaidia kundi la wananchi wa ngazi za chini kwa sababu ugonjwa huu unawakabili rika mbalimbali nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, labda nimwambie kaka yangu kwamba bima ya afya inatoa huduma hiyo, ndio maana katika presentation tuliyowasomea Wabunge, utaona eneo linalotumia fedha nyingi kwenye eneo la bima ni eneo hilo, lakini liawezekana Mbunge anamaanisha Bima ya Afya ya CHF ambayo ndio iko kwenye majimbo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ile bima ya afya ya CHF na tulitaka tuitafute namna ya kuiboresha iweze kuwapa wananchi manufaa mazuri zaidi. Kama ambavyo nimesema kwenye maswali ya nyongeza, kwamba utaratibu ni ule ule. Niendelee kusisitiza Waheshimiwa Wabunge wenzangu, tuendelee kuwa mabalozi wazuri wa bima ya afya kwa watu wote kwa sababu ndipo tutakapoweza kupata suluhisho la kudumu kwa matatizo haya.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: - Je, hadi sasa hali ya ugonjwa wa figo ipoje nchini?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafsi niulize swali dogo la nyongeza. Huu ugonjwa wa figo, ugonjwa ambao unatesa sana, kuanzia sasa hivi mpaka watoto wadogo sana; lakini gharama za matibabu ni kubwa sana. Wakati sasa hivi bima haijaanza kwa nini wasiondoe gharama kwa ugonjwa huu tu, Kwa sababu watu wengi wanakufa kwa sababu ya kukosa pesa ya matibabu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba mlisikia juzi kwenye bajeti yetu kwamba Rais wetu ametoa bilioni tano kwa ajili ya kuwasaidia watu wasiojiweza kwenye eneo hili la matatizo ya figo na mengine. Lakini bado tuna utaratibu mzuri sana kama nchi wa kuweza kuwapa exemption wale ambao hawajiwezi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nafikiri kikubwa ambacho naendelea kukuomba Mheshimiwa Mbunge uwe balozi mzuri wa bima ya afya kwa wote kwa sababu ni suluhisho la kudumu kwenye matatizo haya. Tuna magonjwa mengine hapa ni asilimia 15, hii ni asilimia saba, wanateseka sana watanzania. Kwa hiyo mimi ninachosema tuwe mabaloozi wazuiri wa bima ya afya kwa wote tutapata suluhisho la kudumu kwenye tatizo hili.