Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 29 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 381 2023-05-19

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: -

Je, hadi sasa hali ya ugonjwa wa figo ipoje nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asia Abdukarim Halamga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa utafiti uliofanyika hapa nchini Tanzania katika jamii ulionyesha kuwa asilimia saba ya Watanzania wanaishi na ugonjwa wa figo, ambao kwa kiasi kikubwa unahusishwa na ugonjwa wa shinikizo la juu la damu, ugonjwa wa sukari na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitoe rai kwa wananchi kupima afya mara kwa mara kwani kwa kuchelewa kutambua tatizo la afya madhara yake ni makubwa na gharama ya matitabu inakuwa kubwa.