Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia Wavuvi wa Ziwa Tanganyika zana za uvuvi za kisasa?

Supplementary Question 1

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru nimesikiliza majibu ya Serikali na kwa takwimu alizozitoa Naibu Waziri ni wazi kabisa kwamba bado atujawa na dhamira ya dhati ya kuwasaidia wavuvi wa Ziwa Tanganyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kufahamu ni mkakati upi wa Serikali kwa sasa kwa ajili ya kuwasaidia wavuvi wa Ziwa Tanganyika kwa sababu na ninyi mmekili kuna changamoto ya zana ya kisasa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa wavuvi wa Ziwa Tanganyika wanakabiliana na changamoto nyingi ikiwemo utitiri wa leseni lakini changamoto ya vizimba pamoja na changamoto ya kanuni zilizopo. Mheshimiwa Waziri uko tayari kwenda kukutana na wavuvi uwasikilize ili mtakapo kuja na kauli au na utekelezaji uendane na uhalisia wa Ziwa Tanganyika? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu spika, ahsante sana. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwanza niko tayari kuambana pamoja na yeye Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika kwenda kujionea hizi adha ambazo Mheshimiwa Mbunge anazieleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili; mkakati wa Serikali ni pamoja na kuongeza zana za kisasa najua kwenye suala ya uwiano ndiyo ambalo limeleta changamoto. Lakini mwaka wa fedha ujao tumepanga hivyo hivyo maana yake tutaongeza kulingana na mahitaji ya maeneo husika ikiwemo mikopo, tutaleta vilevile vizimba ili kuongeza sasa wigo mpana wa wavuvi katika ziwa hilo, ahsante sana.