Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 29 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 379 2023-05-19

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia Wavuvi wa Ziwa Tanganyika zana za uvuvi za kisasa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua changamoto za wavuvi zilizopo ikiwemo ukosefu wa zana za kisasa za uvuvi. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga fedha kwenye programu maalum ya mikopo wenye masharti nafuu kutoka Shirika la Fedha Duniani (IMF) kupitia dirisha la extended credit facilities (ECF) kwa ajili ya kuwawezesha wavuvi boti za kisasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutekeleza mpango huo, Serikali inakamilisha taratibu za kutoa boti 158 kwa mkopo kupitia Benki ya Kilimo (TADB) kwa Vyama vya Ushirika 45, Vikundi vya Wavuvi 71 na watu binafsi 43. Aidha, katika Ukanda wa Ziwa Tanganyika jumla ya Vyama vya Ushirika vinne, Vikundi vinne na watu binafsi watano wanatarajiwa kunufaika na mikopo wa boti hizo usiokuwa na riba.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile Serikali kupitia TADB inatoa mitaji kwa wakulima, wafugaji na wavuvi ili kuboresha shughuli zao za maendeleo. Aidha, Serikali inawahimiza wavuvi kujiunga katika vikundi na kuanzisha vyama vya ushirika vya msingi, SACCOS na VICOBA ili waweze kukopesheka na kuweza kununua zana na vyombo bora vya uvuvi.