Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta mbegu mpya za migomba?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza kabisa naomba nimtaarifu Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba hiyo miche ya migomba Hai haijafika kwa hiyo niombe sasa commitment ya Serikali kwa kuwa zao hili ni zao muhimu sana katika Jimbo la Hai ni lini mtatuletea miche mipya ya migomba kuondoa changamoto tuliyonayo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa kuwa zao la mgomba linaenda sambamba na zao la vanila lakini zao la vanila kwa sasa bei imeshuka sana ukilinganisha na ile ya Dunia sasa hivi kilo moja ni shilingi 20,000 lakini inatokana na mazao yanayotokana na vanila inayotoka nje ya nchi yanakuja kwa wingi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuzuia mazao ya vanila yanayotoka nje ya nchi ili zao hili liweze kuongezeka bei hapa Tanzania?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana Mheshimiwa Mbunge ni kwamba kwa kuwa sasa hivi Serikali inaendelea na utaratibu wake wa teknolojia ya chupa kwa maana ya tissue culture kwenye zao la mgomba kama ambavyo ameeleza na anataka commitment ya Serikali kwenye kupeleka miche hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie tu kwamba Serikali itapeleka kulingana na mahitaji ya eneo husika, kwa hiyo kusema lini exactly kwa wakati huu hatuwezi kutaja moja kwa moja lakini tuwahakikishie wananchi wa Hai kupitia Mbunge wao Serikali itapeleka miche katika baadhi ya maeneo ya Jimbo la Hai.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la vanila ni kwamba tumechukua wazo la Mheshimiwa Mbunge Serikali itafanya tathimini ili kuweza kusaidia zao hilo la vanila.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta mbegu mpya za migomba?

Supplementary Question 2

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana nashukuru kwa kunipa nafasi hii nami niulize swali la nyongeza. Kumekuwa na hasara kubwa kwa wakulima wa migomba kwa sababu ya ugonjwa wa mnyauko. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha wanatokomeza ugonjwa huu ili wakulima wa migomba wapate faida? Ahsante sana. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mkakati wa Serikali ndiyo pamoja na hizi tafiti ambazo zinafanyika za kuja na aina mpya ya mbegu ambayo itakuwa na uwezo wa kukabiliana na magonjwa mnyauko na huo ndiyo mkakati sahihi kwa sasa, kwa hiyo tuwahakikishie tu wananchi kwamba Serikali ipo kazini ili kuondoa hii adha ya wakulima ususani katika zao la mgomba.