Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 29 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 378 2023-05-19

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta mbegu mpya za migomba?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa niaba ya Waziri wa Kilimo ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Hai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 Serikali kupitia Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha TARI – Tengeru imefanikiwa kutumia teknolojia ya chupa (Tissue Culture) katika kuzalisha mbegu bora aina ya TARIBAN 1, TARIBAN 2, TARIBAN 3, TARIBAN 4, FHIA 17 na FHIA 23 ambayo ina ukinzani dhidi ya magonjwa (Madoa meusi na Panama (banana wilt) ambayo yamekuwa yakiathiri tija na uzalishaji wa zao la migomba. Uzalishaji wa miche hiyo pia unafanyika kupitia vituo vya utafiti vya TARI – Uyole na TARI – Maruku.

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi kufikia tarehe 30 Aprili, 2023 jumla ya miche 30,000 imezalishwa na kusambazwa kwa wakulima katika Mikoa ya Kilimanjaro miche 5,000, Kigoma miche 9,000 na Kagera miche 9,000. Uzalishaji na usambazaji wa miche hiyo unaendelea ili kuwafikia wakulima katika Mikoa ya Morogoro, Mbeya, Arusha na maeneo mengine yenye fursa ya uzalishaji wa zao la migomba ili kuwezesha wakulima kupanda mbegu bora za migomba na hivyo kuongeza tija na kipato cha mkulima.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika msimu wa mwaka 2023/2024 Serikali kupitia Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania imepanga kushirikiana na maabara binafsi za Crop Bioscience na maua mazuri kuzalisha na kusambaza takribani miche 1,500,000 ya migomba aina ya Grand Nain ambayo itasambazwa kwa wakulima wakiwemo wakulima wa Mkoa wa Kilimanjaro.