Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA K.n.y. MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga na kukarabati Vituo vya Afya ili kuendana na utekelezaji wa Bima ya Afya kwa wote?

Supplementary Question 1

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kwa niaba ya Mheshimiwa Dkt. Charles Kimei. Je, lini Serikali itakarabati kituo cha Mwika Kaskanzini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika maeneo ambayo kuna zahanati, lakini maeneo ni madogo: Je, Serikali ipo tayari kupandisha zahanati za Rombo kuwa vituo vya afya? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza; la kwanza kuhusu lini Serikali itafanya ukarabati wa katika Kituo cha Afya cha Mwika, Serikali itafanya ukarabati katika kituo hiki cha afya kadiri ya upatikanaji wa fedha. Tutaangalia katika mwaka wa fedha 2023/2024 kama kimetengewa fedha ya ukarabati, basi tutahakikisha fedha inaenda mara moja. Kama hakijatengewa fedha kwenye mwaka huu wa fedha, tutahakikisha katika mwaka wa fedha 2024/2025 Kituo cha Afya cha Mwika kinatengewa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali la pili la kupandisha hadhi zahanati kuwa kituo cha afya katika eneo la Rombo, tunalipokea hili kama Serikali. Nichukue nafasi hii kumwelekeza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kufika katika zahanati hizi ambazo zimetajwa na kuangalia kama zinakidhi vigezo vya kupandishwa kuwa vituo vya afya na kuwasilisha taarifa hii katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kuona ni namna gani tunawasaidia wananchi wa maeneo haya kupata vituo vya afya.