Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 29 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 373 2023-05-19

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA K.n.y. MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga na kukarabati Vituo vya Afya ili kuendana na utekelezaji wa Bima ya Afya kwa wote?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Jimbo la Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mpango na mikakati madhubuti ya kujenga na kukarabati vituo vya afya nchini ambapo katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 jumla ya Shilingi bilioni 118 zilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya 236 katika Kata za kimkakati nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuendelea kutekeleza azma ya Serikali ya kuboresha huduma ya Afya nchini, kiasi cha Shilingi bilioni 8.75 kimetengwa katika mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya vipya 15 na ukamilishaji wa vituo vya afya vitano. Vituo hivi vya afya vinapaswa kutoa huduma kwa wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) pamoja Mfuko wa Afya wa Jamii ulioboreshwa (iCHF).