Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga shule ya Bweni ya Wasichana katika Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY J. MAKOA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Pamoja na majibu ya Serikali, Kondoa Girls hii ilikuwa ni Shule ya Kidato cha Kwanza mpaka cha Nne, lakini Serikali ilifanya maamuzi ya kuibadilisha kuwa Kidato cha tano na sita na ikawaondoa wale wa O’level. Sasa Kondoa bado tuna uhitaji wa Sekondari ya Bweni ya Wasichana: Je, ni lini Serikali itairudishia sekondari ambayo waliichukua kujengea sekondari ya wasichana ya bweni ya O’Level?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Wananchi wa Kata ya Bolisa wana hamu ya kuona sekondari yao ya kata inaazwa kujengwa, na tayari kama Halmashauri ya Mji tulipokea barua ya mapokezi ya fedha: Sasa ni lini Serikali italeta fedha ili wananchi wa Bolisa waanze kujenga sekondari yao ya kata?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Makoa, kwanza kutokuwa na shule ya bweni ya wasichana katika Halmashauri ya Mji wa Kondoa, Serikali kwa sasa inaweka nguvu katika kuhakikisha kila mkoa unapata shule moja ya wasichana ya bweni ambayo ni kubwa itakayoweza kuchukua watoto katika mkoa husika na tayari shilingi bilioni 30 ilikuwa imeshatengwa, ambapo shule 10 katika mikoa 10 zimeshajengwa na tunaenda kwenye Phase II ambapo tutajenga tena shule tano. Vilevile tutaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuona Kondoa nao wanapata shule ya bweni ya wasichana ya Kidato cha Kwanza mpaka cha Nne kadiri ya bajeti itakavyoruhusu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la Kata ya Bolisa kupata shule yao ya sekondari, nilijulishe Bunge lako Tukufu kwamba tayari Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI, imeshakamilisha michakato yote ya kuweza kupeleka fedha katika Halmashauri zote 184 nchini kwa ajili ya ujenzi wa shule za sekondari. Muda siyo mrefu Halmashauri hizi 184 zitapata fedha hii kwa ajili ya ujenzi wa sekondari ikiwemo Kata ya Bolisa kule Halmashauri ya Kondoa Mjini.