Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

Idadi ya Shule za Awali Nchi Elimu bora ni uti wa mgongo wa maendeleo ya jamii yoyote ile na ni msingi bora wa elimu kwa watoto unaoanzia toka shule za awali na za msingi:- (a) Je, kuna shule ngapi za awali kati ya mahitaji halisi? (b) Je, ni nini mipango ya haraka kuhakikisha shule za awali zinakuwepo katika shule zote za msingi za Serikali nchini?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kutokana na mwamko ambao umejitokeza hivi sasa kwa watoto wengi kuhudhuria shule kutokana na elimu bure, lakini vilevile kumekuwepo na changamoto mbalimbali yakiwemo pia malalamiko kutoka kwa wananchi.
Je, Serikali inajipanga vipi kuhakikisha kwamba changamato hizi inaziondoa ili watoto wote waweze kupata elimu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, watoto wenye mahitaji maalum bado wao wanakabiliwa na changamoto nyingi; je, Serikali ili kuendana na kasi hii, inajipangaje kuhakikisha watoto wenye ulemavu ambao jamii imekuwa ikiwaficha na wao pia wanapata nafasi ya kupata elimu bure na kuifurahia nchi yao?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika sehemu ya kwanza ni changamoto zinazozikabili shule zetu. Ni kweli mara baada ya mchakato wa Serikali yetu ya Awamu ya Tano, ilipojielekeza kwamba elimu kuanzia shule ya awali mpaka form four kuwa ya bure, tumegundua kuna mambo mengi sana yamejitokeza.
Jambo la kwanza ni kitendo cha watoto wengi waliokuwa wakibaki mitaani kwa kukosa fursa ya kujiunga na shule, hivi sasa wanaende shule. Baada ya hilo kilichotokea ni kwamba tumekuwa na tatizo kubwa la upungufu wa madawati na mambo mbalimbali. Katika hili ndiyo maana Waziri wangu wa Nchi sambamba na Waziri Mkuu walitoa maelekezo kwamba ikifika 30 Juni, madawati yote yawe yameweza kupatikana maeneo ili kuondoa changamoto ya watoto wanaokaa chini. Hata hivyo, Serikali imejielekeza kuhakikisha kwamba tunajitahidi katika ujenzi wa miundombinu ikiwemo madarasa lengo likiwa watoto wote wanaofika shuleni waweze kupata elimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo kuna swali la pili linalohusu watoto wenye ulemavu. Ni kweli mimi mwenyewe nikiri kwamba nimetembelea shule kadhaa za watoto wenye ulemavu, kule Mufindi hali kadhalika pale Dar es Salaam, maeneo hayo nilioyatembelea ni kweli watoto hao wana changamoto mbalimbali, lakini nimeweza kutoa maelekezo mbalimbali kwa Wakurugenzi wa Halmashauri, wahakikishe kwanza watoto hao wenye ulemavu wanapewa kipaumbele. Ndiyo maana katika bajeti yetu ya TAMISEMI mwaka huu tumejielekeza wazi jinsi gani tumejipanga katika suala zima la watu wenye ulemavu ili kwamba watoto wote wanaoenda shuleni kutokana na hali zao wote waweze kupata elimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Amina Mollel, najua kwamba wewe ni mwakilishi halisi na makini sana wa walemavu, tutahakikisha ombi lako hili linafanyiwa kazi katika Serikali hii ya Awamu ya Tano kwa nguvu zote.

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

Idadi ya Shule za Awali Nchi Elimu bora ni uti wa mgongo wa maendeleo ya jamii yoyote ile na ni msingi bora wa elimu kwa watoto unaoanzia toka shule za awali na za msingi:- (a) Je, kuna shule ngapi za awali kati ya mahitaji halisi? (b) Je, ni nini mipango ya haraka kuhakikisha shule za awali zinakuwepo katika shule zote za msingi za Serikali nchini?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri, ni kwa nini sasa katika yale madarasa ya awali ukiangalia fungu lile la elimu bure wanapotoa ile fedha, wale watoto wa madarasa ya awali hawapati ile fedha na inawafanya wazazi waendelee kuchangia yale madarasa ya awali.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema katika majibu yangu ya msingi, ukija kuangalia maeneo mbalimbali ambapo watoto wale wa awali waliokuwa wakienda shuleni, mara nyingi sana walimu waliokuwa wanafundisha utakukuta ni walimu waliokuwa wanachukuliwa mtaani, waliomaliza form four, darasa la saba ambaye anaweza akafundisha. Katika maelekezo ya utaratibu wetu wa elimu, wale watu wote wanaomaliza grade „A‟ wanakuwa na component ya elimu ya awali. Kwa hiyo, utakuja kuona kwamba, wakati mwingine watoto walikuwa wakienda shule wanalazimishwa walipie fedha kwa ajili ya mwalimu wa awali, jambo lile tumesema kwamba, walimu wote sasa hivi wanaomaliza grade „A‟ walimu wale wanaopelekwa mashuleni, kuna mwalimu anayefundisha darasa la awali.
Mheshimiwa Naibu Spika, maelezo yetu kama Ofisi ya Rais – TAMISEMI, ni kuhakikisha Wakurugenzi, wanahakikisha katika allocation ya wale walimu katika shule mbalimbali, wawapeleke walimu ili kusaidia kuondoa ule utaratibu wa wazazi kuwa wanachanga kwa ajili ya kumchukua mtu mtaani kuja kufundisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, hili tumeenda mbali zaidi, ndiyo maana watu walioshudia mwaka jana hapa katika Chuo chetu cha UDOM, tulipeleke takribani walimu wapatao 17,000 katika somo la KKK. Lengo ni kuwawezesha watoto wanapoingia shuleni kuanzia awali na watoto wa darasa la kwanza waweze kujua kusoma na kuandika.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge ni kweli Serikali tunajua changamoto ni nyingi kutokana na suala la elimu bure, lakini Serikali inaangalia jinsi gani tutatatua matatizo mbalimbali. Mara baada ya kufanya jambo hili tumegundua jambo changamoto nyingi zimeweza kujitokeza, changamoto hizi ni kutokana na hii fursa sasa, Serikali ya Awamu ya Tano iliweza kufungua sasa na kupitia hizi changamoto, ndiyo tunaenda kuhakikisha kwamba tunalijenga Taifa la kupata elimu bora. Changamoto hizi, tutakuwa tunazitatua awamu kwa awamu.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri Jafo, ninataka kuongezea kwenye swali alilokuwa analijibu hivi punde kwamba, isichukuliwe kwamba watoto wanaojiunga kwa darasa la awali ni tofauti na watoto wanaoanzia darasa la kwanza mpaka la saba. Wote ni wanafunzi isipokuwa tu wale wana special treatment, lakini fedha inayopelekwa kwa ajili ya uendeshaji wa shule, ndiyo hiyo itumike katika kuendesha na mahitaji ya wale watoto wa awali.
Mheshimiwa Naibu Spika, ingawa tunafahamu Serikali kwamba mahitaji ya watoto wa awali ni maalum sana. Jitihada kubwa itakayokuwa inafanyika ni kuona namna gani tutaongeza hii bajeti, pia kutafuta facilities kwa ajili ya watoto hawa wa awali kwa sababu namna yao ufundishwaji ni tofauti na hawa wengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii tu kuwaomba Walimu Wakuu wa shule na Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya kuhakikisha kwamba hawatenganishi zionekane kwamba kuna shule ya awali na shule ya msingi inayoanzia darasa la kwanza. Hii shule ni moja na ndiyo maana hata walimu wake ni walewale, kwa sababu wale walimu wanaomaliza grade „A‟ wanakuwa wana component ambayo wamefundhishwa namna ya kufundisha watoto hawa wa madarasa ya awali.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

Idadi ya Shule za Awali Nchi Elimu bora ni uti wa mgongo wa maendeleo ya jamii yoyote ile na ni msingi bora wa elimu kwa watoto unaoanzia toka shule za awali na za msingi:- (a) Je, kuna shule ngapi za awali kati ya mahitaji halisi? (b) Je, ni nini mipango ya haraka kuhakikisha shule za awali zinakuwepo katika shule zote za msingi za Serikali nchini?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, mara kwa mara umekuwepo usumbufu wa walimu wa awali kupata mishahara yao kwa wakati.
Je, kuna mkakati gani wa kuwapatia mishahara yao kwa wakati?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri Mheshimiwa Waziri hapa amelizungumza punde kwamba walimu wa awali ni walewale ambao wapo katika utaratibu wa walimu walioajiriwa. Kwa hiyo, ina maana kwamba, hatutarajii mshahara wa mwalimu wa awali uchelewe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, walimu wote wanapata mishahara yao katika utaratibu ule wa kawaida sambamba na walimu wengine katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Isipokuwa inawezekana kama nilivyosema awali katika majibu yangu ya msingi ya mwanzo kwamba inawezekana katika maeneo mengine watu walikuwa wanawachukua walimu kutoka mtaani, kutoka katika mfumo usiokuwa rasmi, ambao wazazi walikuwa wanachangia. Kwa sababu jukumu letu kubwa sasa tumepeleka walimu wengi wa grade „A‟, ili sasa waweze kufundisha yale madarasa ya awali kama ilivyokusudiwa kwa sababu wamepewa ile package ya kufundisha watoto wa awali ili mradi matatizo hayo yote Mheshimiwa Ishengoma yatakuwa hayapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimeona, swali lako lilikuwa makini lakini huo ndiyo utaratibu, ambao tunaenda nao. Lengo letu ni kwamba, watoto wetu wapate elimu bora katika shule zetu.