Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 33 Education, Science,Technology and Vocational Training, Ofisi ya Rais TAMISEMI. 266 2016-05-31

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

Idadi ya Shule za Awali Nchi

Elimu bora ni uti wa mgongo wa maendeleo ya jamii yoyote ile na ni msingi bora wa elimu kwa watoto unaoanzia toka shule za awali na za msingi:-
(a) Je, kuna shule ngapi za awali kati ya mahitaji halisi?
(b) Je, ni nini mipango ya haraka kuhakikisha shule za awali zinakuwepo katika shule zote za msingi za Serikali nchini?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Susan Anselim Lyimo, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, mahitaji halisi ya madarasa ya awali ni 16,014 ambayo ni sawa na idadi ya shule za msingi zilizopo nchini kwa sasa. Shule zenye madarasa ya awali ni 14,946 ambazo ni sawa na asilimia 93.33 ya mahitaji. Hivyo, shule za msingi 1,068 hazina madarasa ya awali.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa vyumba vya madarasa ya awali unafanywa na Halmashauri kwa kushirikisha na nguvu za wananchi kupitia Mpango wa Fursa na Vikwazo yaani O and OD (Opportunity and Obstacle to Development). Azma ya Serikali ni kuhakikisha inajenga na kukamilisha vyumba vya madarasa vya awali kwa shule zote 1,068 zenye upungufu huo. Hivyo nitoe wito kwa Halmashauri zenye mapungufu haya kuangalia upya vipaumbele vyake na kutenga bajeti ya kuwezesha ujenzi wa miundombinu hiyo muhimu.