Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Nangurukuru - Liwale?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kunujibu swali langu kwa ufupi na kwa malengo ambayo niliyakusudia. Ninapenda nishauri barabara hii ianze kujengwa toka Nangurukuru kuelekea Liwale kwa sababu itatengeneza muunganiko wa lami inayotoka Dar es Salaam – Kilwa Masoko pamoja na Mkoani Lindi kuelekea Liwale na kugusa majimbo yote yalipo katika barabara hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba niulize maswali yangu mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kupata kujua;

Je, katika awamu ya kwanza ya ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara hii, itajengwa kilometa ngapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuna barabara ya kutoka Njianne kwenda Kipatimu yenye urefu wa kilometa 50, imekuwa ikijengwa kwa urefu wa mita 700 mwaka 2021, mita 700 2022 na mita 600 2023;

Je, ni lini Serikali itakuja na mradi wa kimkakati ili iweze kujenga kwa urefu mrefu katika barabara hii?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo: -


Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wake wa karibu katika barabara hii. Lakini pia tumeupokea ushauri wake, kwamba ianze kujengwa kutoka Nangurukuru kwenda Liwale, naamini haya tutaweza kuyazungumza. Mkandarasi huyu mmoja anaweza akaanza upande wa Nangurukuru – Liwale ama Liwale – Nangurukuru, yote yanawezekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali yake mawili ya nyongeza, la kwanza anataka kujua ni kilometa ngapi katika ujenzi huu utakaoanza Mwaka wa Fedha 2023/2024; ni kilometa 72 kati ya kilometa 230.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, anataka kujua barabara hii ya Tinga – Kipatimu, ni kweli kwamba barabara hii tumekuwa tukiijenga sisi kama TANROADS kidogokidogo. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaendelea kuijenga barabara hii hadi ukamilifu wake, na sasa tumetenga jumla ya takribani milioni 281.81 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara hii katika Mwaka wa Fedha ujao, 2023/2024, ahsante.