Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 33 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 437 2023-05-25

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Nangurukuru - Liwale?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), inaendelea na kazi ya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Nangurukuru hadi Liwale yenye urefu wa kilometa 230. Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ipo katika hatua za mwisho. Katika mwaka wa fedha wa 2023/24, Serikali itaanza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami kwa awamu ya kwanza, kuanzia Liwale.