Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua migogoro kati ya Wananchi na maeneo ya Hifadhi za Taifa ikiwemo Jimbo la Momba?

Supplementary Question 1

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Nimeyasikia majibu ya Mheshimiwa Waziri, lakini nataka tu kumwambia kwamba, migogoro ipo kwa sababu wananchi wanachukuliwa wanawekwa ndani. Sisi hii tunai-term kama mgogoro. Maswali yangu mawili ya nyongeza ni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri ameshawahi kutuambia tulete maombi Wizarani. Tumeshaleta maombi: Ni lini maombi yetu yatajibiwa ili kuwapa wananchi kipande cha ardhi ili waendelee kuendesha shughuli zao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Je, kama maombi haya yakitoka yatakuwa hapana, Serikali inachukua hatua gani kuendelea kuwasaidia wakulima hawa wapate maeneo ya kulima kwa sababu, ni Watanzania na hawana mahali pa kwenda ili kuendelea kulea watoto wao?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Condester, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa aliwahi kuleta maombi yake na haya maombi mchakato wake unaendelea. Ila kwenye upande wa matokeo ya haya maombi kwamba, yatakuwaje, inategemea sasa na maeneo ambayo sisi tunayaona kama ni ya muhimu, hususan kwenye maeneo ambayo tunatunza vyanzo vya maji na maeneo ambayo ni muhimu kwa kuhifadhiwa. Kwa hiyo, Serikali itafanya tathmini na itaangalia umuhimu wa maeneo haya kwa ajili ya kutunzwa na Serikali na yale ambayo tutaona tunaweza tukayaachia, basi wananchi wataweza kufaidika na maeneo ambayo tutaweza kuyaachia.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua migogoro kati ya Wananchi na maeneo ya Hifadhi za Taifa ikiwemo Jimbo la Momba?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, siku ya tarehe 22 Jumatatu, kumetokea vurugu na sintofahamu kubwa sana kati ya wananchi wa Kijiji cha Jangwani Eneo la Mto wa Mbu na Askari wa Uhifadhi wa Eneo la Ziwa Manyara na kusababisha mwananchi mmoja kufariki na wananchi kadhaa kujeruhiwa kwa risasi za moto: Je, ni kwa nini askari hawa wa uhifadhi wamekuwa wakitumia nguvu kubwa kukabiliana na hii migogoro kati ya wananchi na maeneo ya hifadhi kiasi kwamba, wananchi wanapoteza maisha na wengine wengi kujeruhiwa? Kwa nini kusiwe na njia nyingine mbadala kukabiliana na changamoto hizi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nifafanue kidogo kwa ridhaa yako. Kwa kawaida wahifadhi wanakuwa kwenye maeneo yao ya kutekeleza majukumu yao ya kawaida ya kila siku. Mgogoro huu ulijitokeza katika ziwa Manyara ambapo askari walikuwa katika shughuli zao za doria na waliweza kukamata wahalifu watatu ambao walikuwa wamevamia katika hifadhi hiyo. Baada ya wahalifu hawa kukamatwa ili wafikishwe kwenye vyombo vya kisheria kwa mujibu wa taratibu na sheria zilizopo, wavuvi zaidi ya 30 walijiunga kwa pamoja na wakaenda kuwavamia wale wahifadhi ambapo walikuwa katika maeneo yao ya doria ya kawaida. Kwa bahati nzuri walikuwa tayari wameshawafunga pingu wale wahalifu watatu, lakini wananchi walienda kuwashambulia hao askari. Katika kujiokoa, waliweza kuwaachia hao wahalifu wakakimbia na pingu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilichotaka kusema hapa ni kwamba, suala linapofika kwenye vyombo vya sheria ama wahalifu wanapokutwa na hatia, basi tuache sheria ichukue mkondo wake; lakini inapofika wananchi wanaungana pamoja, wanalishambulia jeshi, jeshi lenyewe sasa linakuwa linaonekana halina nguvu. Kizuri zaidi na kwa kuwa, maelekezo ya Mheshimiwa Waziri yameshaelekeza kwamba tusitumie nguvu, hawa askari waliweza kukimbia na hawakuweza kufanya vurugu yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maandamano hayo, ilisababisha askari kujumuika na wahifadhi ili kuwatawanya watu. Watu walikuwa wengi sana kwa sababu waliungana, ni wanavijiji wa maeneo yale waliwazingira na kufanya maandamano, na walikuwa wanavunja magari, wakikutana na gari wanafanya uhalifu. Kwa hiyo, katika vurugu zile ndiyo zilisababisha sasa huyo mwananchi kufikwa na maafa hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunawaomba sana wananchi wajitahidi sana kuheshimu vyombo vya Dola vilivyopo kwa sababu, viko kisheria na vinatekeleza majukumu yaliyokasimiwa. Kizuri zaidi, hawa tumewakasimisha madaraka kulinda rasilimali za nchi. Kwa hiyo, tunapowashambulia, tunawapunguzia nguvu ya kulinda rasilimali zilizopo hapa nchini.

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua migogoro kati ya Wananchi na maeneo ya Hifadhi za Taifa ikiwemo Jimbo la Momba?

Supplementary Question 3

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi. Kwa kuwa chanzo kikubwa cha migogoro ya wananchi na wanaoishi katika maeneo ya hifadhi na wahifadhi ni mipaka pamoja na alama zinazoonekana, lakini pia ni pamoja na kuzuia matumizi mseto katika maeneo ya WMA kinyume na mikataba iliyofungwa katika uanzishaji wa WMA hizo: Je, Serikali ina mkakati gani mahususi wa kuondoa changamoto hizo ili kuwezesha wananchi kuishi kwa ushirikiano mwema na wahifadhi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kimsingi Serikali inatamani sana kuimaliza hii migogoro, lakini tunatambua kwamba mahitaji ya ardhi sasahivi ni makubwa, wananchi wanaendelea kuongezeka na kila mtu anatamani kumiliki ardhi. Ardhi iliyobaki ni ardhi iliyohifadhiwa ambayo ni inasimamiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii na utalii. Kwa hiyo, kumekuwa na hizi changamoto za hapa na pale na mara nyingi wananchi wanasema ni migogoro, lakini sisi tunasema siyo migogoro kwa sababu, maeneo yana mipaka yake, yana ramani zake, yana GN zake. GN zipo na zinajulikana, isipokuwa pale ambapo kunakuwa na sintofahamu ya mpaka, tunaenda kuufafanua kwa kuweka vigingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naendelea kuwaomba wananchi kwamba sisi tunaendelea kuongezeka, lakini ardhi ni ile ile. Tuendelee kuheshimu haya maeneo kwa mustakabali mzima kabisa wa Serikali na kwa vizazi vinavyokuja. Tunatunza haya maeneo siyo kwa sababu tu yameangaliwa, tunatunza kwa sababu tunaendelea kuongezeka.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua migogoro kati ya Wananchi na maeneo ya Hifadhi za Taifa ikiwemo Jimbo la Momba?

Supplementary Question 4

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ina WMA ya Magingo, lakini uanzishwaji wa TANAPA, ile Hifadhi ya Mwalimu Nyerere imeingia kwenye maeneo ya WMA ya Magingo katika Kitalu cha Nachengo, Kijiji cha Mpigamiti na Ndapata na Kimambi: Je, Serikali inachukua hatua gani kwenda kutatua migogoro hii iliyoletwa na uanzishwaji wa Hifadhi ya Mwalimu Nyerere?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaenda kuufafanua huo mpaka na kutafsiri mpaka ili WMA ziweze kufanya kazi zake na Hifadhi ya TANAPA iendelee na shughuli zake.