Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 33 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 436 2023-05-25

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua migogoro kati ya Wananchi na maeneo ya Hifadhi za Taifa ikiwemo Jimbo la Momba?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa inachukua hatua mbalimbali kutatua migogoro baina ya hifadhi na wananchi. Hatua zinazochukuliwa ni pamoja na kufanya tathmini ya aina, chimbuko na namna ya kutatua migogoro husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) inasimamia misitu minne ya hifadhi katika wilaya ya Momba. Misitu hii ni Isalalolunga, Isalalo, Ivuna North na Ivuna South ambayo kimsingi haina mgogoro na wananchi. Katika kuimarisha ulinzi na usimamizi wa hifadhi hizi, Serikali imechukua hatua mbalimbali za kukabiliana na uharibifu zikiwemo kuweka alama za kudumu za mipaka, kutoa elimu ya uhifadhi kwa jamii, kuondoa wavamizi na kuchukua hatua za kisheria kwa wahalifu.