Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Tarafa za Kitumbeine na Engarenaibor hususan kwenye migodi ya Rubi?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa tarafa ya Kitumbeine na Engarenaibor ziko mpakani pia zina rasilimali nyingi ikiwemo machimbo ya Rubi. Wananchi wa Mundarara kwa nguvu zao binafsi wamejitolea ardhi pia wamejenga Kituo cha Polisi hadi kufikia kwenye ngazi ya lintel.

Je, Serikali haioni haja sasa kuunga mkono wananchi hawa kwa kumalizia kituo hiki cha Polisi ili kulinda usalama wa raia na rasilimali zao? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, tumetambua juhudi za wananchi wa tarafa ua Kitumbeine na Engarenaibor ndiyo maana kwenye jibu langu la msingi nimesema tutawaunga mkono katika bajeti ya mwaka 2023/2024. Labda niwe more pragmatic katika bajeti ijayo tutatenga fedha za kuunga juhudi tuweze kukamilisha jengo lililojengwa kwenye eneo hili. Ahsante sana.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Tarafa za Kitumbeine na Engarenaibor hususan kwenye migodi ya Rubi?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nimehudumu kwenye Kamati hii miaka miwili na nusu, Jeshi letu la Polisi linakabiliwa sana na uchakavu wa muindombinu ya vituo vya Polisi pamoja na makazi ya Askari kote nchini ikiwemo Jimbo la Mbulu Mji Manyara.

Je, ni mkakati upi wa Serikali wa kuondoa tatizo la uchakavu wa majengo ya Askari kote nchini?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA AMAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge kwamba baadhi ya vituo vya Polisi majengo yake ya vituo ni chakavu na nyumba za Askari ni chakavu. Kwa msingi huo Wizara ya Mambo ya Ndani kupitia Jeshi la Polisi limeandaa mpango mkakakti wa miaka 10, kwa ajili ya kufanya ukarabati wa vituo vilivyochakaa na nyumba Askari zilizochakaa, kwa hivyo kama eneo lako Mheshimiwa Mbunge pia lina changamoto hii litafikiwa. Tunashukuru sana.