Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 33 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 434 2023-05-25

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Tarafa za Kitumbeine na Engarenaibor hususan kwenye migodi ya Rubi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali na Mheshimiwa Zaytun Seif Swai, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tarafa ya Kitumbeine na Engarenaibor zipo katika Wilaya ya Longido, Mkoa wa Arusha, Tarafa hizi hazina vituo vya Polisi vinavyofanya kazi. Huduma za Polisi hutolewa kwenye kituo cha Polisi cha Wilaya ya Longido kilichopo kilometa 54 toka Kitumbeine na kilometa 35 toka Engarenaibor. Serikali inatambua juhudi za wananchi wa Tarafa hizo mbili kuanza kujenga vituo vya Polisi viwili kwa nguvu zao na kwa kuwashirikisha wadau.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Tarafa ya Kitumbeine jengo la Kituo cha Polisi limejengwa katika Kijiji cha Gelai Lumbwa, Kata ya Gelai Lumbwa lakini bado hawajaanza ujenzi wa nyumba za makazi ya Askari. Katika Tarafa ya Engarenaibor wananchi wamejenga Kituo cha Polisi katika kijiji cha Mundarara, Kata ya Mundarara na ujenzi umefikia kwenye hatua ya lintel.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inawapongeza wananchi wa Tarafa ya Kitumbeine na Engarenaibor na itawaunga mkono katika kuchangia nguvu za wananchi ili kukamilisha ujenzi wa majengo hayo katika bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 ili kutoa huduma za Polisi katika maeneo hayo. Ahsante.