Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. ROBERT C. MABOTO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itabainisha mipaka ya Kata ya Wariku - Bunda Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, nina swali moja la nyongeza. Kutokana na tatizo hili kuwa kubwa katika Halmashauri ya Mji wa Bunda na hasa kwa sababu kuna kata tatu, nne Kata ya Bunda Stoo, Kata ya Kunzugu, Kata ya Balili na Kata ya Mcharo ambazo zimepakana na Hifadhi ya Mbuga ya Serengeti tatizo ni hili hili. Je, Serikali itakuwa tayari na yenyewe kuweka mipaka kwenye maeneo hayo? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la Serikali kuhakikisha kwamba mipaka yote katika maeneo ya nchi yetu inatambulika vizuri na hizi kata tatu alizozitaja ambazo zinapatikana na Hifadhi ya Serengeti. Kwanza, nitumie nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kumwelekeza Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya hii na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama kufika katika kata hizi na kuangalia mipaka hii kama iko sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama iko sahihi, basi wahakikishe pillar zinazoenda kuwekwa kwenye kata ile ambayo nimetoka kuitaja kwenye majibu yangu ya msingi, basi wahakikishe wanaweka pia pillars katika mipaka hii kati ya kata hizi tatu za Bunda Mjini na Serengeti.