Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 33 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 431 2023-05-25

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. ROBERT C. MABOTO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itabainisha mipaka ya Kata ya Wariku - Bunda Mjini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Robert Chacha Maboto, Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya mipaka kati ya Kata ya Wariku na kata za jirani katika Wilaya za Butiama na Musoma zilianza kutatuliwa kwa njia ya vikao kati ya Mkurugenzi wa Mji wa Bunda na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya ya Musoma na Butiama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya vikao hivyo, wataalam waliweza kuwakutanisha Viongozi wa Mitaa ya Kata ya Wariku na Vijiji vya Kata za Kyanyari (Butiama) na Suguti (Musoma Vijljini) na kutafasiri mpaka huu ardhini na kugundua kuwa sehemu ya Mto Wariku ulimeguka na kuacha njia yake ya asili kutokana na shughuli za kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuwa na suluhu ya kudumu, zitawekwa nguzo ndefu na pana (pillarrs) zinazoweza kuonekana na kila mwananchi. Kazi ya maandalizi ya nguzo hizo inaendelea na itakapokuwa tayari wataalam watarudi uwandani kwa ajili ya kuzisimika.