Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Vituo vya Afya kwenye Kata zilizopo pembezoni mwa Tabora Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu ya Serikali yanaonyesha kwamba hata hiki Kituo cha Afya kilichopo Misha bado hakijakalimika, hivyo wananchi kushindwa kuona thamani ya fedha za Serikali zinazokwenda maeneo hayo na matokeo yake ni kuweza kuwaambia Wakurugenzi wetu wa Halmashauri wamalizie wakati wanajua kabisa mapato yanayopatikana kwenye halmashauri zetu.

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha ili kumalizia kituo hiki ambacho kitasaidia wananchi wa Kata za Ikomwa, Kakola pamoja na Kabila? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; Tabora Mjini ni moja kati ya Majimbo ambayo yana kata nyingi ambazo ziko mbali, watu wanatembea umbali mrefu mpaka kilomita 30 au 40 kufuata huduma za afya kwenye maeneo ya mjini. Je, Serikali haioni sasa umefika wakati wa kuangalia maeneo ambayo yana changamoto za huduma za afya ili kupunguza changamoto hizi hususani kwenye mikoa yetu ya pembezoni? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Hawa Mwaifunga, la kwanza hili la fedha za kumalizia. Ni kipaumbele cha Serikali kuhakikisha kwamba inamaliza vituo hivi Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nikiri hapa mbele ya Bunge lako Tukufu kwamba Kituo hiki cha Afya cha Misha kinahudumia Kata ya Uyui, Kalunde, Misha, Ikomwa na Kabila na hivyo basi Serikali itatafuta fedha na kuhakikisha zinakwenda mara moja kwa ajili ya kwenda kumalizia majengo haya ili huduma iweze kupatikana kwa wananchi wale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili la changamoto hii. Ni kweli katika Manispaa ya Tabora kuna vituo vya afya vitatu ambavyo vimekamilika ambavyo vinatoa huduma kwa wananchi na hiki Kituo cha Misha kikikamilika kitakuwa ni kituo cha afya cha nne na tutaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya vya kimkakati katika Manispaa ya Tabora ili kuhakikisha huduma ya afya inasogea karibu kwa wananchi.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Vituo vya Afya kwenye Kata zilizopo pembezoni mwa Tabora Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Tunaishukuru Serikali kwa ujenzi wa Kituo cha Afya Machwechwe pamoja na changamoto zingine ndogo ndogo nimewasilisha TAMISEMI mara kwa mara juu ya changamoto ya kukabiliana nayo ya gharama kubwa za vifaa vya ujenzi. Sasa je, ni lini Ofisi ya Rais, TAMISEMI watatuongezea fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa kile Kituo cha Afya cha Machwechwe?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaangalia, tutakakaa na Mheshimiwa Amsabi Mrimi kuhakikisha tunaangalia katika mwaka wa fedha huu unaoenda kuanza wa 2023/2024, ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya kumalizia Kituo cha Afya cha Machwechwe kule Wilayani Serengeti na ikiwepo basi tutahakikisha fedha hizo zinaenda mara moja.

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Vituo vya Afya kwenye Kata zilizopo pembezoni mwa Tabora Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika mpango wa Serikali wa kujenga vituo vya afya vya kimakakati, Kata ya Utiri Halmashauri ya Mji wa Mbinga ni moja ya kata ambazo ziliainishwa kujenga kituo hicho. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hiki cha afya? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hiki Kituo cha Afya cha Utiri, Wilayani Mbinga, kama nilivyosema hapo awali Serikali ilitenga zaidi ya bilioni 117 kwa ajili ya ukamilishaji wa vitu vya afya vya kimkakati hapa nchini. Tutaangalia kwamba kituo hiki kama kimetengewa fedha, basi fedha hizo ziweze kwenda mara moja na kuanza kufanya ujenzi ili kutoa huduma kwa wananchi wa Utiri na kama fedha hiyo haijatengwa tutahakikisha bajeti inayokuja nayo, tutakitengea fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa kituo hiki.