Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 33 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 430 2023-05-25

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Vituo vya Afya kwenye Kata zilizopo pembezoni mwa Tabora Mjini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mpango mkakati wa kujenga vituo vya afya katika kata za pembezoni Tabora ambapo katika mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali ilitenga Shilingi Milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Misha. Aidha, ujenzi wa Jengo la OPD na Maabara umekamilika na kituo hicho tayari kimesajiliwa na kimeanza kutoa huduma kwa wagonjwa wa nje, ujenzi wa jengo la wazazi, jengo la upasuaji upo katika hatua za ukamilishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya kwenye maeneo ya kimkakati nchini yakiwemo maeneo ya pembezoni ikijumuisha maeneo ya Jimbo la Tabora Mjini.