Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza majengo katika Kituo cha Afya cha Matamba Wilayani Makete?

Supplementary Question 1

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Rais, kwa sababu ndani ya kipindi cha muda mfupi cha miaka miwili amejenga vituo zaidi ya vinne vya afya ndani ya Wilaya ya Makete kitu ambacho kwa historia ya Wilaya ya Makete hakikuwepo kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa maswali yangu ya nyongeza ni haya swali la kwanza; kuna Kituo cha Afya Kitulo, Kituo cha Afya Bulongwa, Kituo cha Afya Lupalilo na sasa Kituo cha Afya Mbalache hivi vimejengwa, vimekamilika lakini havina vifaa tiba, ipi ni kauli ya Serikali ili vifaa tiba vianze kupelekwa hapa na wananchi wa maeneo yale waweze kuanza kupata huduma kwa ajili ya kuwasaidia? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; kuna Kituo cha Afya cha Ipepo au kwa maana ya eneo la Ipepo, wananchi wale wameandaa tofali zaidi ya laki moja, wameandaa mawe kwa ajili ya kuanza kujenga kituo cha afya. Je, ni upi mkakati wa Serikali kuwasaidia wananchi wa Kata ya Ipepo ili waweze kuwa na kituo cha afya kwa sababu wanasafiri umbali wa zaidi ya kilomita 50 hadi 100 kwenda kufuata huduma ya afya kwenye Jimbo langu la Wilaya ya Makete? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la kwanza la Mheshimiwa Sanga la vifaa tiba, Serikali imetenga fedha katika mwaka wa fedha huu ambao tupo wa 2022/2023, shilingi milioni 450 kwa ajili ya kununua vifaa tiba kwa vituo vya afya vilivyopo Wilayani Makete lakini vilevile kuna shilingi milioni 50 kwa ajili ya zahanati zilizokuwepo katika Wilaya ya Makete.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge na Wanamakete kwa ujumla kwamba kuna shilingi milioni 600 ambayo imetengwa kwenye bajeti ya mwaka 2023/2024, kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba kwenye vituo hivi vya afya ambavyo Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan imejenga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda katika swali lake la pili la lini Serikali itasaidia nguvu za wananchi pale kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Ipepo katika Kata ya Ipepo kule Makete. Ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba inakuwa na vituo vya afya katika maeneo ya kimkakati na hivi Mheshimiwa Mbunge ameitaja hapa kwamba ipo kilomita 50 kutoka Makao Makuu ya Wilaya, basi nichukue nafasi hii kumwelekeza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Njombe kuhakikisha anafika katika eneo hili la Ipepo na kufanya tathmini na kuona kama kituo hiki cha afya kinastahili kupandishwa hadhi sasa kuwa kituo cha afya kamili na walete taarifa yake Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hiki cha afya.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza majengo katika Kituo cha Afya cha Matamba Wilayani Makete?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kata ya Manolo, Halmashauri ya Lushoto wameshajenga Wodi ya Mama na Mtoto na wodi mbili za baba na za akinamama, lakini sasa wako katika ujenzi wa theater. Je, Serikali iko tayari kuunga mkono juhudi hizi za wananchi ili sasa tuweze kukipasisha kiwe kituo rasmi cha afya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la la nyongeza Mheshimiwa Shangazi la Kituo cha Afya Manolo kule Wilayani Lushoto, Serikali itafanya tathimini katika ujenzi huu wa theater ya pale Manolo na kadri ya upatikanaji wa fedha tutahakikisha kwenye bajeti hii tunayoenda kutekeleza kama ipo tutapeleka fedha kuwasaidia wananchi hawa, lakini kama haipo tutatenga katika bajeti ya mwaka 2024/2025, ili kusapoti jitihada zile za wananchi pale.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza majengo katika Kituo cha Afya cha Matamba Wilayani Makete?

Supplementary Question 3

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika Kata ya Mwandoya kuna kituo kikubwa sana cha afya ambacho kinahudumia zaidi ya watu 3,500, lakini kuna upungufu mkubwa sana wa majengo, hakuna jengo la mama na mtoto wala jengo la x-ray. Je, ni lini Serikali itajenga majengo hayo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wake wanapata huduma ya afya iliyo bora hasa Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan na ndiyo maana katika mwaka wa fedha uliopita ilitengwa bilioni 117 ya kuhakikisha kwamba tunajenga vituo vya afya vya kimkakati. Sasa tutaangalia kituo cha afya hiki cha Mwandoya ni namna gani tunaweza tukatafuta fedha kama Serikali ya kwenda kujenga majengo ya mama na mtoto. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza majengo katika Kituo cha Afya cha Matamba Wilayani Makete?

Supplementary Question 4

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Halmashauri ya Bunda inajenga hospitali yake kwenye Kata ya Bunda Stoo na tunatambua Serikali imeshatoa bilioni moja na zinahitajika zaidi ya bilioni tatu ili ile hospitali ikamilike. Je, Serikali ina mkakati gani wa kutoa hizo pesa haraka ili hospitali ikamilike na wananchi wa Bunda wapate mahitaji sahihi na kwa karibu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Mheshimiwa Bulaya alivyokuwa ameshasema, Serikali imeanza kupeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya kule Bunda na tutaangalia katika mwaka wa fedha unaokuja huu wa 2023/2024 ni shilingi ngapi imetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi huu wa Hospitali ya Wilaya na tutahakikisha kama Serikali tunapeleka fedha mara moja kuendelea na ujenzi huo.