Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza: - Je, Serikali imefikia wapi kuhusu mchakato wa pensheni kwa wazee wote?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa mujibu wa sensa, wazee wako asilimia 5.7 tu, idadi hii ni ndogo sana ikilinganishwa na umuhimu na mchango mkubwa wa wazee hawa katika Taifa hili. Je, Serikali haioni haja na umuhimu wa kutenga chanzo kimoja mahususi kwa ajili ya pensheni ya wazee hawa?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni pamoja na upande wa Zanzibar. Kwa kuwa wazee wa upande wa Zanzibar wanapatiwa pensheni kwa wazee wote, ni kwa nini Serikali inachukua muda mrefu wa kufanya utafiti tusijifunze kwa wenzetu wa Zanzibar, japo kuanza na wazee wa umri wa miaka 70 ambao kwa mujibu wa sensa wako asilimia 2.7 tu? Ahsante. (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, wazee kwa mujibu wa sensa ni kweli ni asilimia 5.7, lakini katika kuangalia umuhimu huo wa wazee na ndiyo maana nikasema kwenye jibu la msingi kwamba Serikali itaendelea kufanya utafiti na kuangalia best practice ya uwezekano pia wa Serikali wenyewe kuangalia katika masuala ya kibajeti kama inaweza kuhudumia kundi hili.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, tayari hata ukiangalia kwenye swali lake la pili ambalo linaelezea kufananisha ulinganifu wa upande wa Tanzania Zanzibar, kwamba wazee wamekwishaanza kulipwa, vivyo hivyo, ni mambo yote haya ya kifedha ambayo katika kuangalia lazima tuone namna ambayo tunaweza tukapata fedha za uhakika kuwalipa wazee hawa.

Mheshimiwa Spika, wazee waliokuwa wanafanya kazi wamejumuishwa kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na katika Mifuko hiyo kuna skimu maalum ambayo inaruhusu sasa mtu yeyote, hata akiwa hajaajiriwa, kutoa michango yake katika mifuko hiyo na baadaye kuja kupata pensheni yake.

Mheshimiwa Spika, la mwisho, niseme tu kwamba katika utafiti ambao tunaufanya kwa kipindi hiki, haitachukua muda ili kuweza kuliangalia ikiwa ni zingatio, kama jinsi ambavyo Serikali inatambua mchango wa wazee hawa, umuhimu wao, lakini pia kama chemchemi ya busara na waliochangia kwa sehemu kubwa uchumi wa Taifa. Kwa hiyo tumewaangalia pia na tumeendelea kuweka utaratibu kama huu wa TASAF wa kuwapa fedha ambapo kaya maskini wanasaidiwa wazee hawa, lakini pia kuna taratibu za utoaji wa mikopo ambazo nazo pia zinaendelea.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo wakati haya mambo yanaendelea sambamba na hilo, ni pamoja pia na kujiridhisha sasa kwenye masuala ya kibajeti kama tutaona umuhimu. Tutalileta kwenye Bunge lako Tukufu kwa ajili ya kupata ushauri, maoni na mapendekezo ya wadau, ahsante.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza: - Je, Serikali imefikia wapi kuhusu mchakato wa pensheni kwa wazee wote?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri, kumekuwa na malalamiko kwa baadhi ya wazee katika maeneo mbalimbali wakiwemo wa Mkoa wa Mara, kwamba hawapati ile pensheni yao kwa wakati. Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha wazee hawa ambao wamelitumikia Taifa wanapata pesa yao kwa wakati?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Amos Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, niombe tu kwa sababu hilo ni suala mahususi kabisa la Mkoa wa Mara, niwasiliane na Mheshimiwa Mbunge niweze kupata taarifa za kwa nini ucheleweshwaji unafanyika kwa sababu ni jambo ambalo kwa sasa tunalipa kimtandao na taarifa zinapatikana kwa wakati na tumekuwa tukilipa kwa wakati kabisa katika kipindi hicho. Kwa hiyo jambo hili litakuwa mahususi, nimwombe Mheshimiwa Ester Bulaya anipatie taarifa hizo niweze kufanya ufuatiliaji mara tu baada ya Bunge hili, ahsante.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza: - Je, Serikali imefikia wapi kuhusu mchakato wa pensheni kwa wazee wote?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Hili suala la upande wa Zanzibar kupata pensheni ya wazee wote na Tanzania Bara kukosa wakati ni nchi moja, naomba kujua, nini tamko la Serikali kuhusu wazee wa Bara ambao wanatakiwa kupata pensheni sawa na wazee wa Zanzibar?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere, Mbunge wa Bunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kama nilivyojibu kwenye swali la msingi kwamba kwenye masuala ya kipensheni tayari tunayo Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, kwa hiyo mtu yeyote kwa sasa, hata kabla ya uzee, unaweza ukaanza kupeleka fedha.

Mheshimiwa Spika, katika upande wa pili, kuhusiana na kwamba tutoe tamko; ni hilo la kufanya utafiti ili kuweza kujiridhisha uwezo wa Serikali katika kuhudumia wazee hawa.

Mheshimiwa Spika, tatu, suala hili tayari wazee wanahudumiwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa sasa tunavyo vituo 14 vya wazee wasiojiweza ambavyo ni vya Serikali, vinahudumia hawa wazee na vituo 15 vya watu binafsi na jumla ya wazee 496 wanapata huduma kwenye hayo maeneo.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, Serikali ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, iliweka mpango wa TASAF ambao unanufaisha wazee. Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imeona bado pia kuna umuhimu wa kuwahudumia wazee, imeweka utaratibu wa mikopo, utoaji wa fursa na mitaji; Serikali hii hii imeweza kuendelea kuwaangalia wazee kwa kuwatolea huduma ya matibabu bure na kuna desks zaidi ya 588 kwenye hospitali zetu kwa ajili ya kuwahudumia.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo hili suala Serikali inaliangalia kwa kina sana kuona namna gani wazee wetu tunawaenzi na kuwaheshimu katika mchango mkubwa walioutoa wakati wa ujana wao kuchangia uchumi wa Taifa. Ahsante.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza: - Je, Serikali imefikia wapi kuhusu mchakato wa pensheni kwa wazee wote?

Supplementary Question 4

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wazee wengi ambao walikuwa wafanyakazi wa Shirika la Posta na Simu na ATCL na Mashirika mengine kama Reli, mpaka sasa hivi wanahangaika kupata vipensheni vyao. Je, ni lini Serikali itamalizana na wazee hawa ili wakifa wakapumzike kwa amani?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kifo ni mpango wa Mungu lakini hatuombei itokee hivyo kwa wazee wetu, waishi na waendelee kudumu.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali hilo la Mheshimiwa Asha kuhusiana na wazee hawa waliokuwa watumishi wa Shirika la Posta pamoja na Reli kupata pensheni zao; itakumbukwa vizuri kwamba tayari kulikuwa na mashauri mbalimbali ya wazee ambao walikuwa wanafanya kazi kwenye mashirika hayo. Wapo tayari ambao wamekwishalipwa pensheni zao lakini pia wapo ambao wameendelea kuwa na madai. Hii imetokana zaidi na kutokuwepo kwa taarifa sahihi za madai yale lakini Serikali imeendelea kufanya ufuatiliaji.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimwombe pia Mheshimiwa Mbunge, mama yangu Asha, baada ya hapa pia nipate taarifa ya madai hayo, kama kuna watu specific au mahususi tuweze kwenda kufanya ufuatiliaji kwamba wamekwama wapi katika kulipwa kama walikuwa kweli wafanyakazi halali, ahsante.