Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 32 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 415 2023-05-24

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza: -

Je, Serikali imefikia wapi kuhusu mchakato wa pensheni kwa wazee wote?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, pensheni kwa wazee wote inajumuisha wazee ambao walikuwa katika ajira ambao kwa sasa wanalipwa pensheni na Mifuko waliyochangia wakati wanafanya kazi na pili, wazee ambao hawajawahi kuajiriwa kwa sasa hawalipwi.

Mheshimiwa Spika, mchakato wa kuwalipa pensheni wazee wote ambapo utajumuisha wazee ambao hawajawahi kuajiriwa ni utaratibu mpya ambao utahitaji kugharamiwa na bajeti ya Serikali. Hivyo, itahitaji kufanyika utafiti wa kina ili kuona uwezo wa Serikali katika kulipa pensheni kwa wazee wote. Hata hivyo, kwa sasa Serikali imekuwa inahudumia wazee kutoka katika familia au kaya zenye umaskini uliokithiri kupitia Mradi wa TASAF ambapo wazee ni sehemu ya familia hizo, ahsante.