Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, lini mradi wa kuunganisha umeme wa Gridi ya Taifa kutoka Nyakanazi hadi Kigoma utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Serikali, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza. Serikali inatoa kauli gani ya kutatua changamoto ya umeme mdogo (low voltage) katika Wilaya ya Buhigwe wakati mkandarasi anaendelea na kazi? (Makofi)

Mheshimwa Mwenyekiti, swali la pili. Pamoja na kwamba Gridi ya Taifa imeshaifikia Wilaya ya Kankonko, Kibondo, Kasulu na Buhigwe, bado taasisi za Serikali kama shule, taasisi za kijamii (misikiti, makanisa) pamoja na vitongoji havijapata umeme: Lini Serikali itapeleka umeme? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la umeme hafifu (low voltage) ambalo ameliataja, ni suala la kawaida katika matumizi ya umeme na linatokea pale ambapo watumiaji wanakuwa wengi katika eneo husika, na hivyo vifaa vyetu kuzidiwa. Ni suala kama la kufanya service ya magari. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba TANESCO na Serikali tayari tumetenga fedha kuhudumia maeneo yote yenye matatizo ya low voltage kwa kuongeza vitu vinavyoitwa auto- voltage regulatora na pia kwa kuweka transformer kubwa ili kuweza kusuka umeme mwingi na kuwafikia wahitaji. Katika maeneo anayoyasema nitawasiliana naye ili tujue maeneo mahususi, tuone hatua zilizochukuliwa na zilizofikiwa katika kutatua tatizo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali la pili, ni kweli kwamba Desemba mwaka huu tunatarajia kukamilisha vijiji vyote, lakini tutatafuta fedha kwa ajili ya kupeleka umeme kwenye vitongoji vyote nchini na taasisi zote alizozisema zikiwemo shule, makanisa na maeneo mengine yatapelekewa umeme kufuatia kupatikana kwa fedha, takribani shilingi trilioni tano au sita kwa ajili ya kumaliza maeneo yote yanayohitaji umeme yakiwemo maeneo ya Buhigwe na maeneo mengine ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.