Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 30 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 400 2023-05-22

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: -

Je, lini mradi wa kuunganisha umeme wa Gridi ya Taifa kutoka Nyakanazi hadi Kigoma utaanza?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kavejuru Eliadory Felix, Mbunge wa Buhigwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni habari njema kwamba Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, tayari imeunganisha Mkoa wa Kigoma katika Gridi ya Taifa tangu mwezi Septemba, 2022 kwa kuanzia Wilaya za Kakonko, Kibondo, Kasulu na Buhigwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hatua nyingine kubwa zaidi, hadi kufika mwezi Aprili, 2023, Mkandarasi aitwaye TATA Projects Ltd. amefikia 53% ya utekelezaji wa mradi wa kuunganisha Mkoa wa Kigoma katika Gridi ya Taifa kwa kujenga njia ya kusafirisha umeme yenye msongo wa kilovolti 400 toka Nyakanazi (Biharamulo) mpaka Kidahwe (Kigoma) kwa urefu wa kilometa
280. Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Januari, 2024.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi ya ziada ambayo Serikali inaitafutia fedha ni njia ya kusafirisha umeme (kilovoti 220) ya kutoka Kasulu hadi Buhigwe pamoja na Kituo cha Kupooza Umeme cha Kasulu ambapo thamani ya mradi ni Dola za Kimarekani milioni 20.5. Pia njia ya kusafirisha umeme (kilovolti 220) kutoka Buhigwe hadi Kigoma na Kituo cha Kupooza Umeme cha Buhigwe kwa thamani ya mradi ya dola milioni 19.8 za Kimarekani, ahsante.