Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati majengo ya shule za msingi chakavu Wilayani Masasi yaliyojengwa kati ya mwaka 1905 na 1960?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Namshukuru Mheshimiwa Naibu kwa kutupatia baadhi ya shule chache, kama alivyosema, miongoni mwao zikiwepo Rivango, Chikolopola pamoja na Lulindi Maalum, lakini kama Waziri anavyoona shule zilizokuwa mbovu au chakavu ni nyingi sana kwenye majimbo hayo mawili, hususan kwenye Jimbo la Lulindi anaweza akaona, ziko zaidi ya 20 na kitu. Ni lini atafanya jitihada kwa ajili ya kumalizia hizo shule nyingine chakavu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwambe. Serikali inatambua kwamba, shule nyingi za msingi nchini ni chakavu na tayari tumeona jitihada kubwa za Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutafuta fedha kwa ajili ya kupunguza uchakavu huu katika shule zetu za msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi ambayo ina Jimbo la Mheshimiwa Mchungahela na Mheshimiwa Mwambe, Shule ya Chikolopa imepokea shilingi milioni 331, Shule ya Rivango imepokea shilingi milioni 101, Shule ya Mkalapa imepokea milioni 120, Shule ya Mwena milioni120 na Shule ya Lulindi Maalum imepokea milioni 54. Fedha hizo ni kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa na ukarabati katika shule hizi. Hizi ni jitihada za wazi za Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha upungufu huu wa majengo katika shule za msingi na uchakavu unakwisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwatoe mashaka Waheshimiwa Wabunge, Serikali itaendelea kujitahidi kutafuta fedha hizi kwa ajili ya kukarabati shule nyingi zaidi.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati majengo ya shule za msingi chakavu Wilayani Masasi yaliyojengwa kati ya mwaka 1905 na 1960?

Supplementary Question 2

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika Wilaya ya Itilima kuna shule mbili, shule ya kwanza ni Shule ya Msingi Itubilo ambayo imejengwa mwaka 1965. Majengo yake yamechakaa sana, lakini pia kuna Shule ya Msingi Mwagindu, imejengwa mwaka 1950, nayo majengo yake yamechakaa sana. Je, ni lini Serikali itakarabati majengo hayo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema hapo awali kwamba, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba, inakarabati shule zote ambazo ni za siku nyingi au kongwe katika halmashauri zote nchini. Hivyo basi, Mheshimiwa Mbunge awe na subira, Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kukarabati shule hizi kongwe zilizopo Itilima.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati majengo ya shule za msingi chakavu Wilayani Masasi yaliyojengwa kati ya mwaka 1905 na 1960?

Supplementary Question 3

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nataka kufahamu ni upi sasa mkakati wa Serikali wa kutenga fedha kuweza kwenda kurekebisha shule chakavu kwenye Halmashauri ya Msalala, ikiwemo Shule ya Msingi Isaka, Kata ya Isaka, Shule ya Msingi Kilimbu, Kata ya Mwaruguru na Shule ya Msingi Butegwa, Kata ya Ngaya? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, shule hizi za kule Jimbo la Msalala alizozitaja Mheshimiwa Iddi Kassim zitakarabatiwa kadiri ya upatikanaji wa fedha. Tayari Halmashauri ya Msalala pia imepokea fedha ya kukarabati shule kongwe na chakavu na kujenga shule nyingine kutokana na Mradi wa BOOST ambao fedha zimekwenda. Ni zaidi ya bilioni 230 ambayo Serikali hii ya Awamu ya Sita imetoa kwa kila halmashauri hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kuwaelekeza Wakurugenzi wote wa Halmashauri Nchini, kuhakikisha wanatenga fedha na kuanza ukarabati wa shule chakavu katika maeneo yao ya halmashauri zao kwa sababu, tayari Serikali hii imeshasaidia sana katika ujenzi wa miundombinu mbalimbali kwa kutafuta fedha kutoka Serikali Kuu na wao sasa waanze kutenga kutoka kwenye mapato yao ya ndani.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati majengo ya shule za msingi chakavu Wilayani Masasi yaliyojengwa kati ya mwaka 1905 na 1960?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, Shule ya Mwanhale, Kata ya Mkula, Wilaya ya Busega, majengo yake yamechakaa sana. Je, ni lini Serikali itakarabati majengo hayo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itakarabati shule hizi chakavu zilizokuwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Busega kadri ya upatikanaji wa fedha.