Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 30 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 389 2023-05-22

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: -

Je, lini Serikali itakarabati majengo ya shule za msingi chakavu Wilayani Masasi yaliyojengwa kati ya mwaka 1905 na 1960?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Cecil Mwambe, Mbunge wa Jimbo la Ndanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi ina jumla ya shule za msingi 40 ambazo ni kongwe na chakavu. Kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023 Serikali imepeleka shilingi milioni 200 katika shule kongwe na chakavu za Liloya na Lusonje kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vitano vya madarasa na tayari yamekamilika. Aidha, shilingi milioni 180 zimepelekwa katika Shule Kongwe ya Luatala kwa ajili ya ujenzi wa vyumba tisa vya madarasa, na taratibu za ujenzi zimeanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule nyingine kongwe za Mkalapa, Rivango, Chikoropola, Mwena na Lulindi Maalum zimetengewa fedha kupitia mradi wa BOOST na utekelezaji unatarajiwa kuanza hivi karibuni.