Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Haji Makame Mlenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza: - Je, lini warithi wa Askari E2152 aliyekuwa mtumishi wa Jeshi la Polisi watapewa mafao yao?

Supplementary Question 1

MHE. HAJI MAKAME MLENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza niipongeze Serikali kwa kufikia hatua hii ya kusema Mei, mwezi huu watalipwa warithi wa Marehemu Makame Haji Kheir aliyefariki toka mwaka 2003 lakini kwa sababu ni muda sasa na mwezi Mei ukiisha hajalipwa, ikifika mwezi Agosti nitauliza tena swali hili ndani ya Bunge hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la msingi, kwa kuwa tatizo hili naamini kwamba liko kwa wingi sana Nchini Tanzania. Je, Serikali ina mkakati gani au inawaambia nini Watanzania wenye tatizo kama hili la mirathi ambao hawajalipwa mpaka leo? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu ambayo tumempa Mheshimiwa Mlenge ndio majibu ambayo tunakwenda kuyafanyia kazi. Kwa maana ya kwamba huu mwezi Mei huyu mtu ambaye anadai mafao yake kupitia warithi, atapata mafao yake kwa sababu kila kitu kipo na vielelezo vimekamilika na fedha zimeshatengwa na zipo tayari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado kuna changamoto pamoja na kwamba tunachowaambia Watanzania kwamba madai yote na hiki tunataka tuwaambie, itakapofika Oktoba mwaka huu tutahakikisha kwamba warithi wote wameshapatiwa mafao yao ili lengo na madhumuni sasa changamoto hizi zisiendelee kujitokeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto iliyojitokeza na ndiyo maana tunachukua muda mrefu halafu wananchi wanailaumu Serikali ni kwa sababu ya kuchelewa kuleta vielelezo vitakavyotupa sisi uhalali wa kuweza kuwapatia wananchi ile stahiki. Kwa hiyo niwaombe tu wananchi kwamba likishatokea hili walete vielelezo haraka iwezekanavyo ili na sisi tuweze kuwafanyia haraka waweze kupata haki zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.