Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 27 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 359 2023-05-17

Name

Haji Makame Mlenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza: -

Je, lini warithi wa Askari E2152 aliyekuwa mtumishi wa Jeshi la Polisi watapewa mafao yao?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimwa Haji Makame Mlenge, Mbunge wa Chwaka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mafao ya warithi wa Askari Polisi E.2152 PC Makame Haji Kheir yameshashughulikiwa na Kamisheni ya Polisi Zanzibar, pamoja na Kamisheni ya Utawala wa Jeshi la Polisi, Makao Makuu Dodoma. Mnamo tarehe 8 Machi, 2023, maombi hayo yaliwasilishwa Wizara ya Fedha na Mipango baada ya kukamilika kwa nyaraka zote muhimu zilizokuwa zikihitajika kwa ajili ya malipo ambapo taratibu za uandaaji wa malipo hayo zinaendelea na yanatarajiwa kukamilika ndani ya Mwezi huu Mei ambapo warithi wa Askari huyo watalipwa stahiki zao kwa mujibu wa Sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.