Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali kupitia UCSAF itapeleka minara ya mawasiliano Wilaya ya Malinyi kwa kuwa maeneo mengi ya wilaya hiyo hayana usikivu wa mawasiliano na data?

Supplementary Question 1

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, mpaka hivi ninavyozungumza Ofisi ya Halmashauri ya Malinyi bado hakuna mawasiliano na mkandarasi hajafika site. Hata hivyo ninafahamu kwamba mfuko wa mawasiliano kwa hiyo (UCSAF) walishatoa fedha ila TTCL ambao walipewa kazi hawajafanya mpaka sasa hivi;

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri uko tayari kuambatana na mimi weekend hii wewe au Mkurugenzi wa TTCL na UCSAF kwenda Malinyi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, sehemu kubwa ya Jimbo la Malinyi hasa Kata ya Usangule, Sofi na Itete kwenye vijiji kama Dabadaba hakuna mawasiliano kabisa.

Je, ni lini Serikali itamaliza changamoto hii?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Antipas, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa Serikali iliingia mkataba wa bilioni 10.88 na Shirika la Mawasiliano Tanzania TTCL, ambapo katika fedha hizo zingine zinaenda katika Halmashauri ya Malinyi ambayo ni milioni 320 kwa ajili ya kujenga mnara wa mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie fursa hii kutoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano TTCL kuhakikisha kwamba, pamoja na Halmashauri ya Malinyi na halmashauri nyingine zote 33 ambazo tumeingia nao mkataba wahakikishe wanakamilisha miradi hii ndani ya wakati, kwani kwa kufanya hivyo tutawarahisishia halmashauri kukusanya mapato na vilevile wananchi wataweza kupata huduma ya mawasiliano bila kuwa na changamoto yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kipengele cha pili, kata ambazo Mheshimiwa amezitaja mimi nilifanya ziara na yeye tukiwa pamoja katika jimbo lake; Kata ya Itete katika eneo linaitwa Madabadaba na Usangule, Kilosa Mpepo, yote hayo yameepata watoa huduma katika mradi wetu wa Tanzania ya kidigitali. Kwa hiyo tunaamini kwamba kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais ambayo ameyatoa ni kwamba ni lazima mikataba hii ikatelezwe ndani ya muda ambao tumekubaliana. Kwa hiyo tunaamini kwamba ndani ya miezi tisa mkataba huu ukikamilika wananchi wa eneo la Malinyi watapata huduma ya mawasiliano.