Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 27 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 357 2023-05-17

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali kupitia UCSAF itapeleka minara ya mawasiliano Wilaya ya Malinyi kwa kuwa maeneo mengi ya wilaya hiyo hayana usikivu wa mawasiliano na data?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari napenda kujibu swali la Mheshimiwa Antipas Zeno Mgungusi, Mbunge wa Jimbo la Malinyi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya mwaka wa fedha 2015/2016 na 2020/2021 Kata za Biro, Sofi, Ngoheranga na eneo ilipo Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi zimenufaika na Miradi ya huduma za mawasiliano ya simu kupitia ruzuku ya Serikali. Aidha, ujenzi wa minara katika Kata ya Ngoheranga na eneo ilipo ofisi ya Mkurugenzi inaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia mradi wa Tanzania ya kidigitali imeainisha Kata za Igawa na Njiwa ambazo tayari zimepata mtoa huduma wa kuzifikishia huduma za mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa minara hii ikikamilika itatoa huduma za mawasiliano katika teknolojia ya 3G na 4G.