Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha masomo yatakayoibua vipaji vya watoto kuanzia shule za msingi?

Supplementary Question 1

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka hapo awali tulikuwa na shule ambazo zilikuwa za wananfunzi wenye vipaji maalumu. Shule hizo zilikuwa Kilakala, Loreza, Tabora Boys, Mzumbe, Iliboru na kadhalika lakini hadi sasa hivi hatuzisikii hizo shule zikizungumziwa au tukipata taarifa kwamba performance yake ya vile vipaji vyao maalum vimetumikaje.

Je, Serikali ina mpango gani basi kuziimarisha hizo shule ilikusudi tuone kwamba huu mtaala ambao unatengenezwa sasa hivi wa mali utaweza pia kuwa na tija katika shule hizi maalum?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; tumeona nchi za wenzetu kama Japan na Uchina wanatilia sana mkazo kwenye kazi za stadi, na matokeo yake ni kwamba zile kazi zinazotengenezwa na wanafunzi zinauzwa wakati wakifanya mahafali ya shule na kuwaalika wazazi ili kusudi wanafunzi wale wapate morali kwamba kweli vile wanavyotengeneza vina maana na wawanye wengine wa shule nyingine wapate moyo kwamba kumbe hizi shule za ufundi zina maana.

Je, Serikali ina mpango gani pia kuanzisha utaratibu ambao hivi vifaa vinavyotengenezwa na wanafunzi hawa wanaokwenda kwenye hizi shule za amali zitakuwa zenye thamani ya kuweza kuuzika ili ziongeze kipato kwenye shule hizi wanazofanyia?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kaboyoka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli alichozungumza Mheshimiwa Mbunge. Nimuondoe wasiwasi, shule hizi bado zipo. Kwa upande wa wasichana ni kama alivyozitaja; tuna Shule ya Msalato hapa Dodoma tuna Kilakala ambayo ipo Morogoro. Pia tuna Tabora Girls ambayo ipo kule Tabora. Kwa upande wa wavulana tuna shule ya Kibaha Sekondari, tuna Mzumbe, tuna Ilboru pamoja Tabora Boys.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani jambo kubwa alilolizungumza ni kwamba hazisikiki. Tunaomba tuchukue ushauri wa Mheshimiwa Mbunge twende tukaimarishe ufundishaji. Hizi ni shule zetu ambazo tunasema ni maalum kabisa kwa ajili ya kupokea watoto wenye vipaji na vipawa mbalimbali. Tunaendelea kuzihudumia na kuziimarisha, lakini tunaomba tuchukue fursa hii, tubebe ushauri wako ili twende tukaziimarishe zaidi ili ziweze kujitangaza kama ilivyokuwa zamani, zilikuwa zinavuma sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili amezingumzia suala la zile study mbalimbali. Kwa vile tumesema kwamba sasa hivi tunafanya mapitio ya mitaala, mapitio ya mitaala hii itakwenda kuongeza baadhi ya masomo ambayo yatakwenda kufundisha sanasana stadi mbalimbali hasa kwenye skills.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimezungumzia suala la kuongeza ubora wa vile vitu ambavyo vitakuwa vinazalishwa ili viende vikapate soko, kwa maana ya tuvibiasharishe iwe kama kitega uchumi cha chuo. Tunaomba tubebe ushauri huo; na kwa vile tunapitia mitaala tutakwenda kuchopeka baadhi ya kozi ambazo tutakwenda kuzungumza au tutakwenda kushughulikia zaidi zile study za mikono na kazi za mikono ambazo tutakwenda kuzipeleka sokoni kwa ajili ya kukuza na kuongea vipato na iwe kama miradi kwenye shule zetu.