Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 27 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 356 2023-05-17

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha masomo yatakayoibua vipaji vya watoto kuanzia shule za msingi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia napenda kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa masomo yanayoibua vipaji vya watoto kuanzia ngazi ya elimu ya msingi. Kwa kuliona hilo Wizara ilianzisha somo la sayansi na teknolojia kuanzia darasa la tatu; stadi za kazi pamoja na sanaa na michezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika masomo hayo mada mbalimbali zinazochochea vipaji zinafundishwa. Kwa mfano katika somo la stadi za kazi wanafunzi hujifunza muziki, uigizaji, ufinyanzi na ususi. Katika somo la michezo na sanaa wanafunzi hujifunza michezo sahili, michezo ya jadi, riadha na mpira. Aidha kwa upande wa somo la sayansi na teknolojia wanafunzi hujifunza matumizi ya nishati, majaribio ya kisayansi, mashine na kazi na kuelea na kuzama kwa vitu.

Aidha, Wizara imetoa mwongozo wa ubainishaji na utambuzi wa wanafunzi wenye vipawa na vipaji wa mwaka 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, Serikali kwa sasa inaendelea na mapitio ya mitaala ikiwemo Mtaala wa Elimu ya Msingi ambapo ushauri wa Mheshimiwa Mbunge utazingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.