Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya ukosefu wa Vituo vya Afya katika Jimbo la Tabora Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Tabora Mjini lina kata za mjini na vijini, lakini licha ya kuwa na Hospitali ya Rufaa ya Kitete na hospitali ya wilaya kumekuwa na mrundikano mkubwa wa wagonjwa. Je, nini mikakati ya Serikali kuzisaidia kata za vijijini kupata vituo vya afya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, Sera ya Serikali ni kujenga vituo vya afya kwa kila kata lakini mwaka 2021 Waziri wa TAMISEMI, wakati huo Mheshimiwa Ummy Mwalimu alituletea Wabunge kuandika kata za kimakakati ambazo katika Jimbo la Igalula tuliandika Kata ya Goeko, kizengi na Miswaki.

Je, ni lini mtatekeleza yale maagizo ya kata za kimkakati ili tuweze kujenga vituo vya afya na kusogeza huduma za wananchi katika maeneo hayo? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali lake la kwanza la utofauti wa Mjini na vijijini katika Jimbo la Tabora Mjini na Serikali kusaidia. Serikali itaendelea kutenga fedha kadri ya bajeti ambavyo inaruhusu kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu ikiwemo Jimbo la Tabora Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali la pili la nyongeza la Kata za Goeko, Kizengi na nyinginezo katika Jimbo la Igalula. Serikali itajenga vituo hivi vya afya vya kimkakati kadri ya upatikanaji wa fedha.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya ukosefu wa Vituo vya Afya katika Jimbo la Tabora Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Jimbo la Nkasi Kaskazini lina vituo vya afya vitatu na vinavyofanya kazi ni viwili kati ya kata 17. Ni lini Serikali itajenga vituo 13 vilivyobaki katika Jimbo la Nkasi Kaskazini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hii ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeweka kipaumbele katika kuboresha afya za watanzania na tayari Serikali inatenga fedha katika vituo vya afya kwenye kata za kimkakati pote hapa nchini, ikiwemo kata ambazo amezitaja Mheshimiwa Aida Khenani za kule Nkasi ambayo ina vituo vya afya vitatu tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutangalia katika mwaka wa fedha huu ambao unakwenda kuanza kuutekeleza mwezi Julai, kuona Nkasi imepangiwa vituo vya afya vingapi kwa ajili ya utekelezaji. Kama bado itakuwa haijapangiwa basi Mheshimiwa Mbunge tutaangalia katika bajeti ya 2024/2025 ili tuweze kuwapangia wana Nkasi kupata huduma bora za afya kupitia vituo vya afya.

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya ukosefu wa Vituo vya Afya katika Jimbo la Tabora Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wananchi wa Wilaya ya Kilindi wanatambua jitihada za Serikali za kupeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya. Lakini tunazo kata tatu kwenye vituo vya afya vitatu kwenye Kata ya Jaila, Masagalu na kata ya Maswaki tunahitaji at least milioni mia, mia ili kuweza kumalziia vituo vya afya. Je, ni lini Serikali italeta fedha katika maeneo hayo? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhamira ya Serikali kujenga vituo vya afya katika Mkakati ikiwemo kata za kwa Mheshimiwa Kigua kule Kilindi Kata hizi za Jaila, Masagalu na Mswaki na tutaangalia katika mwaka wa fedha kama zimetengwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo hivi vya afya na umaliziaji. Kama fedha hizo hazijatengwa nimhakikishie Mheshimiwa Kigua katika mwaka wa fedha 2024/2025 ili Jaila, Masagalu na Mswaki ziweze kupata fedha hizi kwa ajili ya umaliziaji.