Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 27 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 351 2023-05-17

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya ukosefu wa Vituo vya Afya katika Jimbo la Tabora Mjini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mwaka wa Fedha wa 2021/2022 Serikali ilitenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya Misha. Aidha, ujenzi wa Jengo la OPD na Maabara umekamilika na Kituo hicho tayari kimesajiliwa na kimeanza kutoa huduma kwa wagonjwa wa nje, ujenzi wa Jengo la wazazi, jengo la upasuaji na jengo la OPD lenyewe upo hatua za ukamilishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya kwenye maeneo ya kimkakati ikiwemo vituo vya afya katika Jimbo la Tabora Mjini.