Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Mradi wa Maji katika Kijiji cha Nkundi – Nkasi Kusini?

Supplementary Question 1

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nina maswali mawili ya nyongeza. Kijiji cha Londokazi, Kalundi na Ntalamila wana changamoto kubwa sana ya maji.

Je, ni lini Serikali itakwenda kuchimba visima ili kuondoa adha hiyo ya maji?

Swali la pili, Jimbo la Nkasi Kusini vipo vijiji karibia 20 mwambao mwa Ziwa Tanganyika ambavyo hakuna barabara na hata hii miradi ya maji na vifaa vinashindwa kufika kule, kwa hiyo wananchi wanaendelea kuteseka wanakunywa maji ya kwenye visima pamoja na mifugo. Je, ni lini na ni mpango gani Serikali kwa kushirikiana na TARURA waweze kuchonga maeneo hayo ili vifaa vya miradi ya maji iweze kufika katika vijiji hivyo ambavyo ni Msamba, Kilambo cha Mkolechi, Izinga, Mbwiza, Lyela, Kasanga, Kasapa, Lupata, Lyapinda, Ninde, Kapumpuli na Kilabu cha Mkolechi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Vincent Mbogo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, uchimbaji wa visima sasa hivi tayari gari liko kwenye mkoa wako na tutakuja kuchimba visima kabla ya mwaka huu wa fedha kuisha. Vifaa vyetu kupitika katika barabara ambayo ni mbovu tutafanya mawasiliano na Wizara husika tutahakikisha mitambo ile inafika kwenye vijiji hivi na vijiji hivi vinaweza kuchimbiwa visima ili waweze kupata maji safi na salama na kufaidi ile azma ya Mama kumtua ndoo Mama kichwani. (Makofi)

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Mradi wa Maji katika Kijiji cha Nkundi – Nkasi Kusini?

Supplementary Question 2

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Mradi wa maji kutoka Kijiji cha Lumea, Kalebezo hadi Nyehunge ulijengwa chini ya kiwango, mabomba yanapasuka na kusababisha maji kukatika. Mheshimiwa Naibu Waziri aliwahi kuahidi kwamba atautembelea mradi huo ili ikiwezekana kuufanyia ukarabati na marekebisho upya.

Je, yuko tayari kutembelea mradi huu ili kujionea yanayoendelea?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Eric Shigongo kuhusiana na mradi huu ambao tayari Mheshimiwa Mbunge tumeongea mara kadhaa alipofika Wizarani, niseme kwamba niko tayari na tutakwenda kuhakikisha maeneo yote ambayo yalipata uharibifu tunayafanyia kazi kwa haraka. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Mradi wa Maji katika Kijiji cha Nkundi – Nkasi Kusini?

Supplementary Question 3

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mradi wa Maji Kyerwa Nyaruzumbula mpaka Kamuli utaanza lini? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu tayari tuna mkandarasi wakati wowote mradi utaanza kufanyiwa kazi. (Makofi)

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Mradi wa Maji katika Kijiji cha Nkundi – Nkasi Kusini?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Ni lini mabomba yaliyosambazwa katika Kata mbalimbali ya Jimbo la Mbagala yataanza kutoa maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chaurembo, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mabomba yaliyosambazwa lazima mwisho wa siku yatoe maji, miradi yetu sisi inapokamilika lazima mwisho wa siku itoe maji. Hivyo nikutoe hofu Mheshimiwa Mbunge maeneo yote ambayo tumeshasambaza unafahamu kazi nzuri ya DAWASA inayoendelea kufanyika, kuna matenki makubwa yameshakamilika na sasa hivi yamebakia kwenye hatua za mwisho kabisa ili yaweze kufikia maeneo yote ambayo tayari yana mtandao.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Mradi wa Maji katika Kijiji cha Nkundi – Nkasi Kusini?

Supplementary Question 5

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Upo Mradi wa Mwabusiga katika Kata ya Kishapu wenye thamani ya shilingi milioni 314, mradi wa maji ya Ziwa Victoria. Mradi huu unatekelezwa chini ya mpango wa force account na uko katika Mfuko ule wa Maji na bahati mbaya kabisa fedha sasa hazijaja. Ziko taratibu za ununuzi wa mabomba na vifaa vingine ambavyo vinahitaji fedha. Sasa lini Serikali itakwenda kuleta fedha na ukizingatia mwaka wa fedha sasa tunakwenda kuumalizia? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kishapu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia mradi huu suala la fedha kila mwezi tunakuwa na mgao. Mheshimiwa Mbunge baada ya hapa naomba tuonane ili mgao unaofuata mwanzoni mwa mwezi Juni tuweze kuupatia fedha.