Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 26 Water and Irrigation Wizara ya Maji 345 2023-05-16

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka Mradi wa Maji katika Kijiji cha Nkundi – Nkasi Kusini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vincent Paul Mbogo, Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kijiji cha Nkundi kinapata huduma ya maji kupitia Mradi wa Maji wa Bwawa la Kawa uliojengwa mwaka 2016. Hata hivyo, huduma ya maji kwenye kijiji hicho ilisimama kutokana na changamoto za kiuendeshaji zilizosababishwa na gharama za kusukuma maji kulingana na uwezo wa wananchi. Katika kukabiliana na hali hiyo, Serikali imechukua hatua ya kuunganisha Chombo cha Watumiaji Maji Ngazi ya Jamii (CBWSO) cha kijiji hicho na vijiji vingine viwili vya Kipande na Kantawa ili kumudu gharama za uendeshaji. Tayari maji yameanza kusukumwa na kazi inayoendelea sasa ni kukarabati mabomba kwenye maeneo yaliyopasuka. Baada ya kazi hiyo, wananchi 4,540 wa Kijiji cha Nkundi wataendelea kupata huduma ya maji.