Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, nini kauli ya Serikali juu ya wateja waliolipia shilingi 27,000 ambao wanatakiwa kulipa fedha zaidi ili kuunganishiwa umeme?

Supplementary Question 1

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Kwanza nimpongese Meneja wa TANESCO wa Wilaya ya Igunga kwa hatua kadhaa ambazo ameendelea kutupa ushirikiano katika kutatua tatizo hili kwa niaba ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; pamoja na changamoto hii ya malipo ilijitokeza, lakini pia kumekuwa na changamoto ya kukatika umeme mara kwa mara pake katika Mji wa Igunga hususan mjini kati pale, maeneo ya Mwamashimba, Igulubi, Nanga, Bukoko, Ikumba na Ikunungu. Je, nini kauli ya Serikali au Serikali ina mpango gani wa kutatua hii changamoto ya dharura ambayo inaathiri shughuli za kiuchumi za wananchi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; ukiangalia katika utekelezaji wa mipango hii ya Serikali pale katika jimbo letu. Kulikuwa na mpango pia wa Serikali kuongeza nguvu kwa kujenga kituo cha kuzalisha umeme. Je, Serikali ina mpango gani katika hili? Ahsante.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI K.n.y. WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mbunge Ngassa kwa sababu ni mfuatiliaji mzuri sana wa miradi ya maendeleo katika jimbo lake. Kuna wakati hata mimi alinichukua kutoka Wizara ya Madini kwenda kumsaidia changamoto za wananchi wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala lake la kwanza, napenda kumjulisha kwamba Serikali imeanza kutekeleza Mradi wa Gridi Imara wenye thamani ya shilini bilioni 500 ambao utakwenda kujenga kwanza vituo vya kupooza umeme katika kila wilaya; pili kujenga njia ya kusafirishia umeme; na tatu kufanya marekebisho makubwa kwenye njia ya umeme ili umeme nchini uwe wa uhakika, lakini pia Bwawa la Nyeyere litakapokamilika nadhani hiyo adha ya kukatika kwa umeme itakuwa ni historia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la pili, kuhusu hawa wananchi ambao anasema waliahidiwa kuunganishiwa umeme, ni kwamba Wizara ya Nishati inaendelea na mchakato na mchakato huo utakapokamilika watafahamishwa, ahsante sana.