Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 26 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 342 2023-05-16

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: -

Je, nini kauli ya Serikali juu ya wateja waliolipia shilingi 27,000 ambao wanatakiwa kulipa fedha zaidi ili kuunganishiwa umeme?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI K.n.y. WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nicholaus George Ngassa, Mbunge wa Igunga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati wa uunganishaji umeme kwa gharama ya shilingi 27,000 kwa maeneo yote ya mjini na vijijini, wateja wengi sana walijitokeza na bei ziliporudi za awali, wateja takribani 80,000 walibaki bila kuunganishiwa umeme na walikwishalipia huduma hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, msimamo wa Serikali uliotekelezwa na TANESCO ulikuwa ni kuwaunganishia umeme wateja wote waliolipia shilingi 27,000 bila kuongeza malipo yoyote. Hadi kufikia tarehe 30 Aprili, 2023, wateja wote waliolipia shilingi 27,000 kabla ya Januari, 2022 walikwishaunganishiwa umeme bila kulipa gharama za ziada, ahsante sana.