Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga vivuko ili kuweza kupita magari, pikipiki na baiskeli katika Reli ya Bandari Isaka - Msalala?

Supplementary Question 1

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kumekuwa na changamoto kubwa ya vivuko ambavyo vinasababisha mkwamo wa kutoka kitongoji kimoja kwenda kingine. Kuna changamoto kubwa sana kutoka Kijiji cha Itogwamolo kwenda Kijiji cha Bandari, lakini hivyo hivyo kutoka kitongoji cha Shilabela kwenda Isaka Stesheni na hivyo hivyo kutoka kwenye Kata ya Isaka kwenda ya Jana. Sasa swali langu la kwanza; ni lini Serikali itaweza kutenga fedha ili iweze kujenga vivuko vitakavyowawezesha wananchi kufika kwenye maeneo hayo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa kumekuwa na changamoto kubwa katika eneo la Isaka hasa kwenye suala la bandari.

Je, ni lini sasa Mheshimiwa Naibu Waziri atakuja kwenye Kata ya Isaka ili aweze kufanya mkutano wa hadhara awasikilize wananchi wa Isaka kero kubwa ambayo inayozuka katika maeneo haya ya bandari, ahsante. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wa karibu sana masuala ya kivuko katika eneo hili. Serikali itaanza ujenzi katika vijiji hivyo alivyovitamka vyote, hususan katika Kijiji cha Isaka na Isakajana, Isaka Stesheni na Kitongoji cha Shilabela na Kijiji cha Itogwa hadi Kijiji cha Bandari. Tutaanza ujenzi wa kuunganisha vijiji hivi tarehe 27 ya mwezi huu wa tano.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kwenda kukagua, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na yeye, mara baada ya kuanza ujenzi tutaenda kukagua eneo hili pamoja na eneo la Stesheni ya Kisaka, ahsante.