Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 26 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 341 2023-05-16

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga vivuko ili kuweza kupita magari, pikipiki na baiskeli katika Reli ya Bandari Isaka - Msalala?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mpango wa kuimarisha usalama katika maeneo yote ya makutano ya reli na barabara kuu kwa kujenga madaraja au kuweka mageti ya kisasa yanayojifungua na kujifunga yenyewe ili kuzuia watumiaji wa barabara kupita pale treni inapopita kwenye makutano.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kuweka mageti hayo katika makutano yote ya reli na barabara yaliyopo kwenye barabara kuu yakiwemo makutano ya Isaka. Kwa sasa Serikali imeweka walinzi eneo hilo kwa saa 24 ili kuhakikisha usalama wa watumiaji wa barabara hiyo, ahsante.