Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga barabara ya Kibaoni – Majimoto hadi Inyonga kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Serikali, wananchi wa Mkoa wa Katavi hususan wa eneo hili wamekuwa wakizunguka umbali mrefu kupitia Eneo la Mpanda mpaka Inyonga kutokana na kwamba barabara hii kipindi cha masika imekuwa haipitiki kabisa.

Swali la kwanza; je, Serikali haioni sasa umuhimu wa haraka wa kufanya ujenzi wa barabara hii? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Serikali inafanya ujenzi wa Barabara ya kutoka Mpanda – Uvinza mpaka eneo la Lulafe. Je, ni lini Serikali itakamilisha kilometa zilizobaki mpaka Uvinza ili tuweze kuunganishwa na wananchi wa Mkoa wa Kigoma kwa ujenzi wa kiwango cha lami? Ahsante. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara hii aliyoitamka ni kilometa hizo 60 ambazo zinahitaji kujengwa kwa kiwango cha lami, lakini Serikali iliona umuhimu kwanza kwa kuanza ujenzi wa Daraja la Kavuu ambalo lilikuwa la chuma sasa tunakwenda kuweka zege na kazi hii inaendelea. Katika mwaka wa fedha sasa tutakamilisha hizo kilometa zilizobaki.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kwa Barabara hii ya Mpanda – Uvinza; barabara hii ipo na mkandarasi anaitwa CHICO na tayari tumeanza ujenzi wa kiwango cha lami kilometa 25 na tunategema kwamba mkataba huu utaisha baada ya mwaka mmoja na miezi sita. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa maeneo hayo yote, kwamba Serikali ya Chama cha Mapinduzi inaendelea kutekeleza mradi huu na utakamilika kwa wakati, ahsante. (Makofi)

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga barabara ya Kibaoni – Majimoto hadi Inyonga kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, barabara ya Kwa Sadala – Isuke kilometa 15 imekuwa ni ahadi ya muda mrefu kwamba itajengwa kwa kiwango cha lami na hii ni ahadi ya Mheshimiwa Rais; je, ni lini sasa barabara hii ya Kwa Sadala – Isuke kilometa 15 itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kuhusiana na barabara hii ya Kwa Sadala – Isuke na kwa kuwa ni ahadi za viongozi wetu wa Kitaifa kama nilivyokwishajibu swali la Mheshimiwa Martha kwamba, ahadi zote za viongozi wa Kitaifa, sisi Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi tumeziweka katika mpango wa bajeti ijayo. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge apitishe bajeti itakayosomwa hapa tarehe 22 na 23 ili barabara hiyo iwe sehemu ya utekelezaji huo, ahsante.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga barabara ya Kibaoni – Majimoto hadi Inyonga kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Chombe – Igonda – Kaoze mpaka Ilemba? Ahsante. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bupe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii aliyoitamka kadri Serikali itakavyopata fedha, tutakwenda kuitekeleza barabara hii.

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga barabara ya Kibaoni – Majimoto hadi Inyonga kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Wananchi wa Mkoa wa Songwe wana changamoto wanapokwenda kuhitaji huduma kutoka mkoani imewalazimu kwenda kupitia Mkoa wa Mbeya na kuanza usafiri kuelekea Mkoa wa Songwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mkakati gani wa kujenga Barabara kutoka Mloo – Isasa – Magamba mpaka Mkwajuni ili kurahisha huduma kwa wananchi wa Wilaya ya Songwe? (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyotamka Mheshimiwa Mbunge iko katika mpango wa Serikali wa kujenga na sasa tunatafuta fedha ili tuanze ujenzi wa barabara hii, ahsante.