Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 26 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 340 2023-05-16

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga barabara ya Kibaoni – Majimoto hadi Inyonga kwa kiwango cha lami?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Martha Festo Mariki, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Kibaoni – Majimoto hadi Inyonga yenye kilometa 162. Hadi sasa jumla ya kilometa 9.3 zimejengwa kwa kiwango cha lami sehemu ya Inyonga kilometa 4.2 na Majimoto kilometa 2.6 na Usevya kilometa 2.5 ambapo ni Makao Makuu ya Halmashauri ya Mpimbwe. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuendelea na ujenzi kwa sehemu iliyobaki, ahsante.